TRA

TRA

Wednesday, July 19, 2017

Trump na Putin walifanya kikao cha siri G20

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Rais wa Marekani Donald Trump alikutana na mwenzake wa Urusi Vladmir Putin katika mkutano wa pili wa siri ambao haukutajwa ulipofanyika katika kikao cha mkutano wa mataifa ya G20, imebainika.

Walifanya mazungumzo baada ya mkutano wao wa kwanza lakini ukulu ya White House haijatoa maelezo kuhusu kile kilichozungumziwa.

Rais Trump amekana madai ya kufanyika kwa mkutano huo wa siri na Putin na kusema ni ''habari bandia''.
Uhusiano wa viongozi hao wawili unachunguzwa kufuatia madai kwamba kampeni ya Trump ilishirikiana na Urusi.


 Rais wa Marekani Donald Trump alikutana na mwenzake wa Urusi Vladmir Putin katika mkutano wa pili wa siri

Wapelelezi wa Urusi wanaamini kwamba Urusi ilimsaidia bwana Trump kushinda uchaguzi wa mwaka jana kitu ambacho Urusi imekana.
Bwana Trump amepinga madai kama hayo.
Mkutano wa pili ulifanyika wakati wa chakula cha jioni cha viongozi katika kikao hicho cha G20 mjini Hamburg mapema mwezi huu
Rais wa Marekani alikuwa pekee na Putin alikuwa na mkalimani wake huku vyombo vya habari vya Marekani vikisema kuwa mkutano huo ulichukua saa moja.
Madai ya kilichozungumzwa yaliwasilishwa kwa maafisa wa Ikulu ya Whitehouse na bwana Trump mwenyewe kwa kuwa hakukuwa na wasaidizi wakati wa mkutano huo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger