Mkuu wa
Jeshi la Polisi nchini, IGP Saimon Sirro, amefanya mabadiliko ya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa
wa Shinyanga.
Katika
mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Suzan Salome Kaganda amekuwa Mkuu
wa kitengo cha Mafao na Fidia Makao Makuu ya Polisi, na nafasi yake
inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo
ambaye alikuwa kamanda Polisi Mkoa wa Shinyanga.
Aidha,
Nafasi ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga imechukuliwa na
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Sylverius Haule, ambaye alikuwa
Afisa Mnadhimu wa Polisi wa Mkoa wa Mara.
Uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya Jeshi la Polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.
Imetolewa na:
Barnabus D. Mwakalukwa - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.
SHARE
No comments:
Post a Comment