TRA

TRA

Friday, July 14, 2017

Watu wanaokunywa kahawa wanaishi miaka mingi: Utafiti

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

 
Ukikunywa vikombe vitatu vya kahawa kwa siku unaweza kuishi miaka mingi, kwa mujibu wa utafiti uliofanyiwa karibu watu nusu milioni kutoka nchi 10 za Ulaya.


 Watu wanaokunywa kahawa wanaishi miaka mingi: Utafiti

Utafiti huo uliochapishwa kwenye jarida na Annals of Internal Medicine, unasema kuwa unywaji wa kahawa unaweza kuongeza maisha ya mtu.
Lakini wataalamau wanasema kuwa ni vigumu kusema kuwa ikiwa ni unywaji kahawa unachangia watu kuishi miaka mingi au ni maisha ya kiafya wanayoishi wanywaji kahawa.
Watafiti kutoka shirika la Agency for Research on Cancer and Imperial College London, wanasema wamegundua kuwa unywaji wa kahawa nyingi unahusiana na hatari kidogo ya kufariki hasa kutokana na magonjwa ya moyo.
Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Watu wanaokunywa kahawa wanaishi miaka mingi: Utafiti
Waliafikia uamuzi baada ya kuchunguza takwimu kutoka kwa watu walio na umri wa zaidi ya miaka 35 kutoka nchi 10 za Ulaya
Waliawauliza watu wakati wakianza utafiti kuhusu kiasi cha kahawa walikuwa wakinywa kisha wakaangali vifo vilivyotokea katika kipindi cha miaka 16.
Lakini cha kuvunja moyo kwa wanywaji wa kahawa, ni kuwa ugunduzi huu haueleweki vyema.
Kwa mfano haukuonyesha ni kipato cha kiwango gani wanywaji pombe hupata ikilinganishwa na wale wasiokunywa kahawa.
Huenda ikawa labda watu walio na uwezo wa kununu vikombe vitatu vya kahawa kila siku wana pesa zaidi, na kwa njia moja au nyingine huwasaidia kulinda afya zao.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger