TRA

TRA

Friday, July 21, 2017

YANGA KUMUUZA MSUVA MILIONI 300 MOROCCO, KILA KITU SAFI BADO VIPIMO VYA AFYA TU

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM WINGA wa Yanga SC, Simon Msuva atakwenda Morocco wiki ijayo kufanya vipimo vya afya katika mpango wa kujiunga na klabu ya Ligi Kuu nchini humo, Difaa Hassani El-Jadida kwa ada ya uhamisho ya dola za Kimarekani 150,000 zaidi ya Sh Milioni 300 za Tanzania.
  Difaa ambayo tayari imekwishamchukua Mtanzania mwingine, winga pia Ramadhani Singano ‘Messi’ kutoka Azam FC iko tayari kutoa dola 150,000 kumnunua Msuva ambaye amebakiza miezi tisa katika mkataba wake Yanga.
  Msuva alishindwa kuondoka jana kwenda Kigali, Rwanda na kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kwa ajili ya mchezo wa marudiano Raundi ya kwanza kuwania tiketi ya Faianli za Ubingwa wa Mataifa wa Afrika (CHAN), zinazohusisha wachezaji wanaocheza nchini mwao pekee, ili kushughulikia safari yake Morocco.
Simon Msuva atakwenda Morocco wiki ijayo kufanya vipimo vya afya kuelekea uhamisho wake wa dola 150,000 kwenda Difaa Hassani El-Jadida 
Na baada ya kukamilisha taratibu zote, Msuva ameondoka Dar es Salaam kwenda Kigali kuungana na Stars kujaribu kupata matokeo mazuri ugenini baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Mwanza Jumamosi.
  Baada ya mchezo na Amavubi mjini Kigali Jumamosi, Msuva aliyejiunga na Yanga mwaka 2012 kutoka Moro United, anatarajiwa kwenda moja kwa moja Morocco kwa ajili ya vipimo vya afya ambavyo akifuzu atasaini mkataba mnono.
  Timu hiyo yenye maskani yake mji wa El Jadida ikiwa inatumia Uwanja wa El Abdi inataka kujaribu kutwaa taji la Ligi Kuu ya Morocco, inayojulikana kama Botola, moja ya Ligi bora kabisa barani Afrika.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger