TRA

TRA

Monday, August 28, 2017

Bongo Hapo Zamani: Ndimara Tegambagwe

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Image may contain: one or more people
Ndugu zangu,
Miaka hiyo tuko Primary na Sekondari tulikuwa tukiwasoma waandishi mahiri na wengine wenye majina ya kutisha, ni wakongwe aina ya Ndimara Tegambwage, John Rutayisingwa, Stanley Kamana na wengineo.
Kwenye maktaba yangu ninaye mkongwe Ndimara Tegambwage. Huyu kila tukikutana lazima tubishane kwa hoja. Napenda kumchokoza ili nipate kuchimba madini yaliyo kichwani mwake.
Moja ya kumbukumbu zangu ni usiku ule pale Kinondoni zilipokuwa ofisi za gazeti la Mwanahalisi. Nilifika mahali hapo kama saa moja usiku. Nilikuwa na kawaida ya kufika hapo kukutana na kusalimiana na ndugu zangu kwenye habari.
Pale chumba cha habari niliwakuta ndugu yangu Saed Kubenea, Jabir Idrissa na Mwalimu na Mzee wangu Ndimara Tegambwage. 
Haikuchukua muda tukaanza kubishana kwa hoja mimi na Ndimara juu ya hoja ya kama gazeti lina jukumu ya kuandika yaliyo mazuri pia ya Serikali au chochote kizuri kinachofanywa na Serikali ni wajibu wake na haina haja ya kusifiwa. Tulibishana sana na nikavuna mengi kutoka kwa Mwalimu wangu Ndimara.
Siku mbili baadae, mahali hapo hapo katika muda kama huo, kukatokea tukio la kusikitisha la Saed Kubenea na Ndimara Tegambwage kushambuliwa na wasiojulikana na hata Kubenea kujeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa tindikali machoni.
Binafsi nimemsoma Mwalimu wangu Ndimara tangu nikiwa Sekondari pale Tambaza. Si wengi wenye kujua, kuwa Ndimara alipata kuwa mwandishi wa magazeti ya Chama, Uhuru na Mzalendo.
Si wengi pia wenye kujua, kuwa Ndimara aliasisi gazeti lake lililoitwa 'Radi'.
Na si wengi wenye kujua kuwa Ndimara alipata kuwa Mweka Hazina wa NCCR Mageuzi na hata akawa mbunge kwa muhula mmoja.
Mwalimu wangu Ndimara anazijua harakati za siasa za upinzani, na anaifahamu vema media ya nchi hii.
Tukibaki kwa Ndimara kama Mwanahabari, hakika, enzi hizo Radi ilikuwa radi kweli kweli. Ilishuka mara moja kwa mwezi. Ilipopiga Radi ya Tegambwage hata Ikulu ilitikisika.
Nakumbuka toleo namba moja la Radi lilikuwa na habari kuu yenye kichwa cha habari mithili ya radi;
"Kutawaliwa Kama Kondoo Sasa Basi..!" Hiyo ilikuwa radi haswa iliyoshuka Ikulu ya Mzee Mwinyi!
Nina mengi ya kusimulia ya wakati huo tukisoma magazeti aina ya Radi, Moto Moto, Family Mirror, Fahari, Michapo, Wasaa, Mshindi, Mizani hadi Sauti Ya Siti!
Maggid,
Iringa.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger