TRA

TRA

Monday, August 28, 2017

KESI YA MASOGANGE YAENDELEA TENA LEO KISUTU

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo August 28, 2017 imepokea taarifa ya Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyoonesha kuwa sampuli ya mkojo wa Agnes Gerald maarufu kama Masogange una chembechembe za dawa za kulevya.

Taarifa hiyo imepokelewa baada Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kutoa uamuzi wake ambapo amesema Mahakama imepokea taarifa hiyo na pingamizi la utetezi limetupiliwa mbali.
Pingamizi la upande wa utetezi ni kwamba fomu zilizopelekwa kwa Mkemia Mkuu hazikufuata sheria.
Hakimu Mashauri amesema Mkemia huyo Elia Mulima ambaye ni Shahidi wa kwanza ana haki ya kuandaa ripoti, kupima sampuli na kutoa ripoti Mahakamani.
Kuhusu hoja ya kuwasilishwa maombi ya kupimwa mkojo Masogange, Hakimu amesema ni wazi Polisi walipeleka maombi kwa Mkemia na mshtakiwa alienda akiwa chini ya askari wawili, ambapo walipatiwa kontena kwa ajili ya kuweka sampuli ya mkojo wa Masogange.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger