Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akitambulishwa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 37 wa SADC kwenye ukumbi
wa OR Tambo mjini Pretoria, Afrika ya Kusini. Picha na Ofisi ya Makamu
wa Rais.
Rais
wa Zambia Mhe. Edgar Lungu akiwashukuru washiriki wa mkutano huo wakati
wa Utambulisho kwenye ufunguzi wa mkutano wa 37 wa SADC kwenye ukumbi
wa OR Tambo mjini Pretoria, Afrika ya Kusini.# Picha na Ofisi ya Makamu
wa Rais
Mkutano
huo wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Troika Mbili ya SADC (SADC
Double Troika Summit),unawakilishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzaia Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia Dkt John Pombe Magufuli.Katika mkutano
huo Tanzania itakabidhi nafasi ya Uenyekiti kwa Mwenyekiti mpya.
Double Troika inahusisha nchi wanachama sita ambao kwa sasa ni Swaziland, Tanzania, Afrika Kusini, Angola, Botswana na Msumbiji. Katika mkutano huo Mfalme Mswati III wa Swaziland atakuwa ndiye Mwenyekiti. Ajenda kuu katika Mkutano huu ni kupokea na kujadili taarifa kuhusu hali ya kisiasa, kiulinzi na kiusalama katika Kanda na hasa nchini DR Congo na Lesotho.
Double Troika inahusisha nchi wanachama sita ambao kwa sasa ni Swaziland, Tanzania, Afrika Kusini, Angola, Botswana na Msumbiji. Katika mkutano huo Mfalme Mswati III wa Swaziland atakuwa ndiye Mwenyekiti. Ajenda kuu katika Mkutano huu ni kupokea na kujadili taarifa kuhusu hali ya kisiasa, kiulinzi na kiusalama katika Kanda na hasa nchini DR Congo na Lesotho.
SHARE
No comments:
Post a Comment