TRA

TRA

Monday, August 28, 2017

Mbappe kukamilisha usajili kwenda PSG

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mshambuliaji wa Klabu ya Fc Monaco, Kylian Mbappe anatarajiwa kukamilisha usajili wake wa mkopo na klabu ya Ufaransa Paris Saint-Germain (PSG).

Mchezaji huyo anatarajiwa kutua nchini Ufaransa siku ya Jumatatu, kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya Ufaransa.

Kituo cha redio cha Ufaransa siku ya Jumapili kiliripoti kuwa PSG wamekubali kulipa euro milioni 180 ambazo sawa na dola za marekani 215,000,000) ikiwa ni pamoja na mafao kwa mshambuliaji huyo mwenye miaka 18.
 Kylian Mbappe (kulia)
Usajili huo utaweka historia katika uhamisho kuwa usajili wa pili wa gharama kubwa zaidi katika soka baada ya Neymar, ambaye alijiunga na PSG kutoka Barcelona kwa euro milioni 222 mapema mwezi huu.
Hata hivyo kuna wasiwasi zaidi kuhusiana na kile kilicho juu ya mkutano wa UEFA wa Fedha unaohusu gharama kubwa katika usajili wa wachezaji Fair Play (FFP) na ndio maana PSG wanataka kwanza kumsajili kwa mkopo Mbappe .
Monaco na PSG siku ya Jumapili zilifikia makubaliano ya Kylian Mbappe kwenda PSG kwa gharama ya usajili wa euro milioni 180.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger