Katibu
Tawala wa Mkoa wa Dododma Rehema Madenge akifungua mafunzo ya siku
nane kwa wataalamu wa Afya, Mipango na Fedha kutoka Mikoa Mitano chini
ya ufadhili wa mradi wa Uimarishaji Mifumo (PS3)
SERIKALI
kuanzia sasa inaweza kuokoa zaidi ya Sh Bilioni tisa ambazo zilikuwa
zikutumiwa na maofisa wake mbalimbali katika uandaaji wa mipango na
bajeti katika Serikali za mitaa na Halmashauri kufuatia kuanza kwa
matumizi ya mfumo mpya wa uandaaji mipango na bajeti utakaotekelezwa
chini ya mradi wa uimarishaji wa mifumo ya sekta za umma (PS3). Anaandika Mroki Mroki wa DAILY NEWS Digital.
Mradi
wa PF3 unatekelezwa na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa (TAMISEMI) chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa
la Marekani (USAID). BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa watazindua Mfumo mpya
wa kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa (PlanRep),
Mratibu wa Mfunzo hayo, ambaye pia ni Mtaalaam wa Mifumo ya Tehama na
Mawasiliano kutoka PS3, Desderi Wengaa, alisema katika mfumo wa zamani
uliokuwa unatumika ulikuwa ukiwafanya watendaji wa serikali kutumia muda
mrefu na gharama kubwa kuandaa mipango na bajeti zao lakini huu wa sasa
utaokoa muda na gharama ambazo zinazidi bilioni tisa kila mwaka.
“Mradi huu kupitia mfumo wa PlanRep utasaidia san asana kuokoa gharama
kwaa maana ya rasiliamali fedha zilizokuwa zinatumiwa na serikali
takribani Sh milioni 60 kwa kila halmashauri na zaidi ya Sh bilioni nane
hadi tisa au kumi kwa nchi nzima kwa kutumia mfumo huu ambao pia
utawawezesha watendaji kufanya kazi za kutoa huduma katika maeneo yao
badala ya kuzunguka katika vikao vya kuandaa bajeti,” alisema Wengaa.
Washiriki wa Mafunzo hayo ya namna ya kutumia Mfumo
mpya wa kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa
(PlanRep),wakifuatilia hotuba za ufunguzi zilizokuwa zikitolewa na
viongozi wa mradi pamoja na mgeni rasmi ambaye alikwa Katibu Tawala wa
Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge.
Washiriki wa Mafunzo hayo ya namna ya kutumia Mfumo
mpya wa kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa
(PlanRep),wakifuatilia hotuba za ufunguzi zilizokuwa zikitolewa na
viongozi wa mradi pamoja na mgeni rasmi ambaye alikwa Katibu Tawala wa
Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge.
Mwakilishi wa washiriki wa Mafunzo hayo, Dk Aisha Mahita akitoa neno la Shukrani kwaniaba ya washiriki wote.
Miongoni
mwa wakufunzi wa mafunzo hayo ni timu ya kitaifa ya wakufunzi kutoka
TAMISEMI, Sekretarieti za Mikoa, Wakala ya Serikali Mtandao (Ega), Ofisi
ya Raisi Menejimenti na Utumishi wa Umma, Wizara ya Fedha na Mipango,
PS3 pamoja na wizara zingine ikiwemo Wizara ya Afya.
Zaidi
ya watumiaji 1,500 watafundishwa juu ya mfumo wakiwakilisha ngazi tatu
za Serikali. Mafunzo haya yanajumuisha Maafisa Mipango, Wahasibu,
Wachumi, Maafisa Tehama na Makatibu wa Afya wa Halmashauri.
Mradi
wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3), ni Mradi wa miaka
mitano unaotekelezwa katika mikoa 13 na Halmashauri 93 za Tanzania bara.
PS3 inafanya kazi katika sekta mbalimbali ili kuimarisha mifumo ya
mawasiliano, utawala bora, fedha na rasilimali watu, hususani kwa jamii
zenye uhitaji.
Meza kuu katika picha ya pamoja
SHARE




















No comments:
Post a Comment