TRA

TRA

Saturday, August 5, 2017

Upinzani wadai uvamizi katika Ofisi yao

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Siku tatu kabla ya uchaguzi mkuu kuandaliwa nchini Kenya, muungano wa upinzani umeishutumua serikali kwa kuvamia moja ya ofisi zake. 

Msemaji wa muungano huo anasema kuwa wanaume waliokuwa wamefunika nyuso zao walibeba kompyuta, simu za mkononi na vitabu. 



Lakini serikali imesisitiza kuwa hakuna uvamizi uliofanyika. Mgombea wa upinzani Raila Odinga amesema kuwa atakubali tu kushindwa ikiwa uchaguzi utakuwa wa haki. 

Rais wa sasa Uhuru Kenyatta pia naye ameahidi kuheshimu matokeo ya uchaguzi huo wa siku ya Jumanne licha ya kila mmoja kusisitiza kuwa ataibuka mshindi.

Uchaguzi wa Kenya mara nyingi umekubwa na ghasia. Zaidi ya watu 1000 waliuawa wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger