TRA

TRA

Sunday, September 10, 2017

Angalia mambo ya Diamond

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
            Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amelamba shavu nono la kuingia mkataba wa kibiashara na kampuni ya vinywaji vikali ya Luc Belaire ya nchini Ufaransa. Kupitia ukurasa rasmi wa Instagram wa kampuni hiyo imethibitisha kuwa

Diamond Platnumz atakuwa mwanafamilia mpya kwenye kuitangaza bidhaa hiyo na kuungana na Mastaa kibao duniani ambao pia ni mabalozi wa bidhaa hiyo akiwemo Rick Ross. Baada ya taarifa hizo rapa kutoka Marekani Rick Ross, nae pia alimkaribisha Diamond Platnumz kupitia ukurasa wake wa

                    Instagram kwa kuandika ‘Self Made Tastes Better’ caption iliyoambana na picha ya Diamond Platnumz . Dili hilo ambalo bado halijawekwa wazi ni kiasi gani Diamond Platnumz ataingiza baada ya kusaini na kampuni hiyo, lakini huenda likawa ni dili la mamilioni ya fedha kwani Rick Ross ambaye pia ni Balozi wa Belaire anakadiriwa kulipwa kiasi cha Dola milioni 4.1, zaidi ya Tsh bilioni 8.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger