TRA

TRA

Friday, September 15, 2017

DEREVA WA MBUNGE JOHN HECHE AVAMIWA, AKATWA MAPANGA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
               Dereva huyo akiwa amelazwa hospitali baada ya kujeruhiwa. DEREVA wa Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, John Heche (Chadema) amevamiwa na watu wasiojulikana kisha kumkata kwa mapanga usiku wa kuamkia leo majira ya saa 2 usiku huku ikielezwa kuwa hali yake si nzuri. Ndugu na marafiki wakimjulia hali hospitalini hapo.

Taarifa hizo za kusikitisha zimethibitioshwa na Bosi wa Dereva huyo ambaye ni Mbunge John Heche kupitia Katibu wake,Mrimi Zablon ambaye amekiri kuwa dereva huyo anayefahamika kwa jina la Suez Daniel maradufu ni kweli amepata shambulio hilo na sasa yupo hospitali akipatiwa matibabu. Mbunge, John Heche.

                   TAARIFA KWA UMMA Jana majira ya saa mbili usiku dereva wa mbunge John Heche anayejulikana kwa jina la SUEZ DANIEL MARADUFU alivamiwa na watu wasiojulikana na kushambuliwa kwa kukatwa katwa na mapanga kichwani na hali yake si nzuri, anaendelea na matibabu kwenye Hospitali ya Bomani Tarime. Ofisi ya Mbunge Jimbo la Tarime Vijijini 15/9/2019.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger