TRA

TRA

Friday, September 15, 2017

Kenyatta ampa gari mbunge mwenye umri mdogo

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Mbunge wa umri mdogo zaidi nchini Kenya amekabidhiwa gari ambalo alikuwa ameahidiwa na Rais Uhuru Kenyatta.

John Paul Mwirigi, 23, ambaye ni mbunge wa Igembe Kusini, takriban kilomita 200 mashariki mwa jiji la Nairobi, alichaguliwa akiwa bado mwanafunzi wa chuo kikuu.

Bw Mwirigi alitumia baiskeli na pikipiki za kusafirisha abiria, maarufu kama bodaboda, kuwafikia watu wakati wa kampeni.
Nyingi za pesa alizotumia wakati wa kampeni alizipokea kutoka kwa wahisani.
 Mwirigi akikabidhiwa ufunguo wa gari na Rais Kenyatta
Wakati wa kuapishwa, alitumia magari ya uchukuzi wa umma, kufika majengo ya Bunge jijini Nairobi.
Wabunge walipoalikwa ikulu, alipewa lifti na mbunge mwenzake.
Hata hivyo, wakati wa kuondoka, alitumia gari la uchukuzi wa umma maarufu kama matatu.
„Nimetimiza ahadi yangu kwa mbunge kijana wa Igembe Kusini John Paul Mwirigi katika ikulu ndogo ya Sagana," umesema ujumbe kwenye ukurasa wa Facebook wa Rais Kenyatta.
Picha za mbunge huyo akikabidhiwa gari hilo zimepakiwa kwenye ukurasa huo wa Rais.
John Paul Mwirigi ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu Somo la Ualimu katika Chuo Kikuu cha Mt Kenya alitangazwa mshindi baada ya kupata kura 18,867 na kumshinda mpinzani wake wa karibu Rufus Miriti wa chama cha Jubilee chake Rais Kenyatta, ambaye alikuwa na kura 15,411.
Wagombea wengine, ambao wamekuwa wanasiasa kwa muda mrefu walikuwa ni Mwenda Mzalendo aliyepata kura 7,695, Kubai Mutuma (6,331) na Raphael Muriungi (2,278).
"Niliota nilikuwa nikitoa hoja katika bunge wakati nilikuwa kidato cha tatu. Ndio wakati nilianza kuwauliza wanafunzi wenzangu kunifanyia kampeni kwani ningehitaji kura zao mwaka 2017. Nimeshikilia nafasi za uongozi shuleni na nyumbani," alisema Bwana Mwirigi.
Mwirigi alisema ajenda yake ya kwanza itakuwa kusaidia shughuli za biashara ya kilimo, kukuza ujasiriamali na kulea vipaji.
"Kwa kuwa mimi ninatoka kwenye familia maskini, ninaelewa maswala yanayoathiri wakazi. Ajenda yangu muhimu itakuwa kubadilisha maisha ya watu," anasema.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger