TRA

TRA

Sunday, September 10, 2017

REFA WA KWANZA MWANAMKE ALIYEWEKA REKODI ULAYA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
              Jumapili ya September 10, 2017 muamuzi wa kike wa mchezo wa mpira wa miguu Bibiana Steinhaus ameandika rekodi mpya barani Ulaya kwa kuwa muamuzi wa kwanza wa kike kuwahi kuchezesha mechi ya Ligi Kuu Ujerumani Bundesliga.

         Bibiana Steinhaus mwenye umri wa miaka 38 ameweka rekodi ya kuwa muamuzi wa kwanza wa kike katika Ligi tano kubwa barani Ulaya (Ufaransa, Hispanai, England, Ujerumani na Italia) kuwahi kuchezesha mechi za Ligi Kuu za wanaume.

                   Mchezo wa Hertha Berlin dhidi ya Werder Bremen wa Bundesliga uliyochezwa leo na kumalizika kwa sare ya 1-1, ulichezeshwa na Bibiana Steinhaus ambaye nje ya urefa ni askari Polisi, mchezo wa leo ndio mkubwa wa wanaume aliyowahi kuuchezesha.

Bibiana ameanza kazi ya uamuzi toka mwaka 2007 hadi kufikia hapo amechezesha michezo zaidi ya 80 ya Ligi daraja la pili, amechezesha fainali ya wanawake ya Champions League 2017 na michuano ya wanawake yaOlympic 2012 London lakini tegemea kuendelea kumuona Bundesliga wa 2017/2018 akichezesha mechi kadhaa.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger