Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii
Bw. Patrick Golwike akizungumza na Maafisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa
Dodoma katika kikao kilichofanyika ukumbi wa manispaa ya Dodoma, tarehe
16 Sept, 2107.
Mratibu wa Masuala ya Maendeleo
ya Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bibi Mwajina Lipinga (kulia)
akifafanua masuala mbalimbali kuhusu utendaji kazi wa Ofisi ya Rais
TAMISEMI kuhusu uratibu wa majukumu ya Maendeleo ya Jamii nchini kwa
Maafisa Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Dodoma katika kikao kilichofanyika
kwenye ukumbi wa manispaa ya Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera
na Mipango Bw. Atupele Mwambene akizungumzia masuala mbalimbali ya
Kisera kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Dodoma katika kikao
kati ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Maendeleo ya jamii
wa mkoa wa Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa manispaa ya Dodoma.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Serikalini(HGCU) Bw. Erasto Ching’oro(kulia) akitoa maelezo ya
upatikanaji wa Sera na machapisho mbalimbali zinazohusu masuala ya
Maendeleo ya Jamii kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Dodoma
katika kikao baina ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii na Maafisa
Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Dodoma kilichofanyika kwenye ukumbi wa
manispaa ya Dodoma.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa
wilaya ya Bahi Bw. Mchapa Edward akiomba ufafanuzi kuhusu masuala ya
kiutendaji katika kikao kati ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii na
Maafisa Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Dodoma kilichofanyika katika
ukumbi wa manispaa ya Dodoma.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa
wilaya ya Mpwapwa Bw. Njovu Mikidadi akitoa maoni kuhusu masuala ya
kiutendaji katika kikao kati ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii na
Maafisa Maendeleo ya Jamii wa mkoa wa Dodoma kilichofanyika katika
ukumbi wa manispaa ya Dodoma.
Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka
wilaya ya Chamwino Bi. Sophia Swai akitoa maoni yake katika kikao kati
ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa
mkoa wa Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa manispaa ya Dodoma.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa
wilaya ya Chemba Bi. Flora Shija akitoa maoni yake katika kikao kati ya
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Maendeleo yaJamii wa mkoa wa
Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Dodoma.
Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka
mkoa wa Dodoma wakimsikiliza Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii Bw.
Patrick Golwike(hayupo Pichani) wakati wa kikao cha kujadili masuala ya
sekta ya Maendeleo ya Jamii kilichofanyika katika ukumbi wa manispaa ya
Dodoma.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii
Bw. Patrick Golwike akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa kutoka
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto, Mratibu wa
Masuala ya Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wakuu wa
Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri za Mkoa wa Dodoma mara baada
ya kikao cha kuhamsha ari ya kushiriki kazi za maendeleo katika kikao
kilichojumuisha Maafisa hao kwenye ukumbi wa manispaa ya Dodoma.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW
……………………………………………………………………………
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jamii
Bw. Patrick Golwike amewapongeza maafisa Maendeleo ya Jamii nchini kwa
ujumla kwa kazi wanazofanya kwa ajili ya jamii katika kuamsha ari kwa
wananchi katika kujileta maendeleo.
Ameyasema hayo wakati akizungumza
na Maafisa Maendeleo ya Jamii katika kikao cha kujadiliana masuala
mbalimbali yahusuyo maendeleo ya jamii nchini.
“Niwashukuru sana maafisa
Maendeleo ya Jamii kwa kazi nzuri wanazofanya katika jamii hasa katika
kuamsha ari ya wananchi kujitolea katika kujiletea maendeleo” alisema
Bw. Golwike.
Ameongeza kuwa suala la maendeleo
ni la kila mmoja katika jamii na kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii
kusaidia katika kuamsha ari zaidi ya wananchi kujitolea katika kujiletea
maendeleo.
Kwa upande wake Mratibu wa
Masuala ya Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bibi Mwajina
Lipinga amesema kuwa bado kuna fursa ya kufanya zaidi ya wanachokifanya
kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii katika maendeleo yao ya kazi.
“Bado tunahitaji kujituma zaidi
katika kazi, tufanye kazi na kutimiza majukumu yetu ya kazi kama Maafisa
Maendeleo ya Jamii” alisema Bibi. Mwajina.
Ameongeza kuwa ni muhimu kwa Maafisa Maendeleo ya jamii kutekeleza majukumu yao haswa kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Jamii.
Naye kwa upande wake Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Bw. Atupele Mwambene amesema kuwa
Wizara inayafuatilia na kuyafanyia kazi masuala yote ya Sera yahusuyo
Maendeleo ya Jamii.
Mmoja wa Maafisa Maendeleo ya
Jamii kutoka Wilaya ya Chamwino Bi. Sophia Swai ameishukuru Wizara na
kuiomba iendelee kushirikiana nao katika kutekeleza Sera ya Maendeleo ya
Jamii kwa manufaa ya Jamii.
Sekta ya Maendeleo ya Jamii ni
Sekta muhimu sana katika Ustawi wa jamii na katika kuletea maendeleo ya
mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
SHARE
No comments:
Post a Comment