Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akifungua mkutano
wa kujadili utekelezaji wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la
Afrika kati ya Tanzania na Afrika Kusini leo mjini Dodoma.
Mkurungenzi Mkuu wa Kazi za Umma
kutoka Afrika Kusini Bw. Mziwonke Dlabantu akitambulisha timu ya
wataalamu kutoka nchi hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kujadili
utekelezaji wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika kati ya
Tanzania na Afrika Kusini leo mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Mkutano Balozi
Christopher Liundi akitoa utaratibu utakaotumika wakati wa mkutano wa
wataalamu kutoka Tanzania na Afrika Kusini wakati wa ufunguzi wa mkutano
wa kujadili utekelezaji wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la
Afrika leo mjini Dodoma.
Baadhi ya wataalamu wakifutatilia
ufunguzi wa mkutano wa kujadili utekelezaji wa Programu ya Urithi wa
Ukombozi wa Bara la Afrika kati ya Tanzania na Afrika Kusini leo mjini
Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa katika
picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano wa kujadili utekelezaji wa
Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika kati ya Tanzania na
Afrika Kusini leo mjini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiongea na
waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano wa kujadili
utekelezaji wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika kati ya
Tanzania na Afrika Kusini leo mjini Dodoma.
(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma)
………………………………………………………………………………….
Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, DODOMA
Watanzania wametakiwa kutunza,
kulinda na kuimarisha amani na heshima iliyopo nchini kwani amani hiyo
huifanya Tanzania iheshimike na Mataifa mengine.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel
wakati akifungua mkutano wa kujadili utekelezaji wa Programu ya Urithi
wa Ukombozi wa Bara la Afrika kati ya Tanzania na Afrika Kusini
unaofanyika mjini Dodoma.
Prof. Elisante amesema kuwa suala
la kutunza na kulinda amani iliyopo huanzia kwa wananchi wenyewe,
hivyo, ili Tanzania iendelee kuheshimika ni buni kutunza na kulinda
heshima na utamaduni uliopo kwani amani na heshima, vikitoweka huchukua
muda mrefu kuijenga au kuirejesha.
“Tanzania imeendelea kuheshimika
na kuimarika kwa amani na utulivu uliopo, hivyo sisi kama watanzania
tunahitaji kuitunza, kuheshimu na kuimarisha amani iliyopo kwani suala
la heshima huanzia ndani” aliongeza Pro Elisante.
Akizungumzia mkutano huo, Prof.
Elisante amesema kuwa mkutano huo unalenga kuwa na mazungumzo kati ya
nchi mbili za Tanzania na Afrika Kusini kabla ya kuelekea Mkutano wa
Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC), hatua hiyo inatokana na Afrika Kusini kuwa na maudhui ya kipekee
ya jinsi Tanzania ilivyoshiriki katika ukombozi wa Bara la Afrika
ikiwemo Afrika Kusini.
Prof. Elisante ameongeza kuwa
lengo lingine la mkutano huo ni kuweka historia ili kizazi kijacho
kitambue ushiriki wa Tanzania katika ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo
Afrika Kusini.
Aidha, lengo la Programu hiyo ni
kutambua umuhimu wa Vyama vya Ukombozi katika harakati za kulikomboa
Bara la Afrika na kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na Tanzania katika
kusaidia kwa hali na mali harakati za ukombozi wa Bara la Afrika.
Zaidi ya hayo, Prof Elisante
amesema kuwa Tanzania imefaidika katika nyanja mbalimbali ikiwemo
kisiasa, Kiuchumi na Kiutamaduni ambapo kisiasa Tanzania imeendelea
kuheshimika ndani na nje ya Bara la Afrika hatua inayopelekea kuongeza
pato la Taifa kutokana na utalii unaofanyika katika maeneo ya kihistoria
yaliyotumika wakati wa harakati za Ukombozi wa Bara la Afrika.
Kwa upande wake Mkurungenzi Mkuu
wa Kazi za Umma kutoka Afrika Kusini Bw. Mziwonke Dlabantu amesema kuwa
timu hizo zimekutana kuimarisha uhusiano uliopo kati ya Tanzania na
Afrika Kusini ili kujadiliaana na kuimarisha namna bora ya kutekeleza
Mradi wa Ukombozi wa Bara la Afrika pamoja na kutembelea baadhi ya
maeneo yaliyotumika wakati wa Ukombozi wa Bara la Afrika ikiwemo Afrika
Kusini.
Wadau wanaoshiriki mkutano huo
kutoka Tanzania na Afrika Kusini wizara na taasisi mbalimbali kutoka
pande zote mbili ikiwemo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
ambao ndio waratibu wa program hiyo, Wizara Fedha, Ofisi ya
Rais-TAMISEMI, Maliasili na Utalii, Ulinzi, Elimu, Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Utalii, Habari na Utamaduni kutoka
Zanzibar pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na
Utamaduni (UNESCO).
Programu hiyo ina wajibu wa
kukusanya, kuweka kumbukumbu, kuhifadhi na kukumbuka nakishi ya Urithi
wa Afrika tangu harakati za kupigania Uhuru wa Afrika hadi Bara zima
lilipokombolewa.
Mkutano huo unafanyika mjini
Dodoma kwa muda wa siku tatu ambapo umegawanyika katika makundi matatu
ukihusisha Wataalamu wa Programu, Makatibu Wakuu kutoka katika Wizara
zinazohusika katika utekelezaji wa program hiyo pamoja na Mawaziri
husika katika Wizara hizo.
SHARE
No comments:
Post a Comment