TRA

TRA

Sunday, November 5, 2017

DK. KIGWANGALLA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA ZIWA MANYARA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akisalimiana na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Manyara, Noelia Myonga alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. (Picha na Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii)


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga (wa pili kushoto) kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi na utalii endelevu nchini alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha. (Picha na Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii).



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akigusa maji ya moto ya asili ambayo ni kivutio cha kipekee cha utalii kilichopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. Maji hayo yanakadiriwa kuwa na nyuzi joto 80 ambapo imeelezwa kuwa baadhi ya watalii huweza kuchemsha mayai katika maji hayo. Nyuma yake anayeshuhudia ni Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga. (Picha na Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii).

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger