TRA

TRA

Sunday, November 5, 2017

TBL ilivyoshiriki matembezi ya kusomesha wauguzi wakunga

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



matembezi amref 3
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Samia Suluhu Hassan
matembezi amref 5
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL katika matembezi ya AMREF ya kuchangisha fedha za kusomesha wauguzi fani ya ukunga
matembezi amref 6
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wakifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Samia Suluhu Hassan
………………………………………………………………..
 Kampuni ya TBL Group imeshiriki kudhamini matembezi ya  kuchangisha fedha za kusomesha wauguzi wakunga yaliyoandaliwa na  Shirika lisilo la kiserikali la AMREF yaliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kuongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Samia Suluhu Hasan,ambapo pia baadhi ya wafanyakazi walishiriki katika matembezi hayo.
Akiongea baada ya kumalizika matembezi hayo juu ya kampuni kushiriki,Meneja Mawasiliano wa TBL,Zena Tenga,alisema kampuni inao mkakati wa kusaidia na kushirikiana na wadau mbalimbali wanaofanya jitihada za kuunga mkono zitihada za serikali katika kupambana na changamoto mbalimbali za kijamii.
“Tunawapongeza AMREF kwa kuona umuhimu wa kulivalia njuga suala la kusomesha  wauguzi fani ya ukunga  kwa kuwa  kwa kiasi kikubwa tukiwa na wakunga wa kutosha wenye utaalamu kutaaidia kupunguza  idadi ya vifo vya wanawake wajawazito na watoto wachanga wakati wa kujifungua.
Tenga alisema kuwa TBL itaendelea kuunga mkono jitihada hizi kama ambavyo imeamua kuvalia njuga changamoto nyingine za kijamii  hususani katika kuboresha sekta za elimu na afya nchini.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger