Ikiwa ni
wiki amabayo ya Malaria Duniani, Mataifa mbaliombali Duniani hutumia
nafasi hii kufanya shughuli mbali mbali katika kuadhimisha wiki na siku
ya Malaria duniani.
Kampuni
ya Bima ya AAR imetembelea Hospitali ya Amana iliyoko Ilala Dar es
salaam na kutoa msaada wa vyandarau kwa wamama wajawazito katika
kutimiza lengo la kupunguza uenezi wa gonjwa la Malaria.
Akiongea
na wandishi Habari Hospitalini hapo, Afisa Mahusiano wa kampuni ya bima
ya AAR, Bibi Amisa Juma alisesema, “Tukiwa kama wadau wa Afya Tanzania,
ni jukum letu katika jamii kuonyesha mfano wa kupambana na maradhi
mbalimbali ikiwemo hili Malaria.
Hii
imakua ni utamaduni kwa kampuni ya Bima ya AAR kuadhimisha siku ya
Malaria Duniani kwa kushirikiani na Jamii katika shughuli mbali ikiwemo
kuchangia kutoa elimu juu ya kujikinga na tiba pamoja na kuchangia
matibabu kwa jamii tofauti ya Tanzania. Almalizia Bibi Amisa.
Wafanyakazi wa AAR walitembelea hodi ya kina na mama wajawazito na watoto na kutoa msaada huo.(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment