Mwili wa Papa Wemba wasafirishwa DRC
Mamia ya
watu wamekongamana nje ya uwanja wa ndege wa Kinshasa kuupokea mwili wa
mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka Abidjan
Mwanamuziki
huyo ambaye ametajwa kuwa mmoja ya waanzilishi wa muziki wa kizazi
kipya cha Soukous anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne baada ya mwili huo
kuwekwa katika uwanja wa mpira kwa raia kutoa heshima zao za mwisho.
Maafisa
wa serikali na wanadiplomasia watahudhuria ibada ya kumkumbuka
mwanamuziki huyo katika uwanja wa ndege kabla ya mwili huo kupelekwa
katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Marehemu Papa Wemba
Tamasha
la bure la usiku kucha lilifanyika mjini Abidjan ambapo mwanamuziki huyo
alianguka alipokuwa akiimba.Mwanahabari wa BBC Tamasin Ford anasema
kuwa mashabiki wengi walivalia nguo nyeusi na kubeba mishumaa ili kutoa
heshima kwa nguli huyo wa muziki.
Mkewe Papa Wemba na wasaidizi wake pia walikuwepo.BBC
SHARE
No comments:
Post a Comment