TRA

TRA

Sunday, August 21, 2016

Makamu mpya wa rais wa Sudan Kusini azuru Khartoum

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



media
Makamu mpya wa rais wa Sudan Kusini Taban Deng Gai
Makamo wa raisi mpya wa Sudani Kusini Taban Deng Gai ameanza ziara ya siku mbili mjini Khartoum kujadili masuala nyeti ambayo bado hayakufanyiwa kazi tangu Sudan kaskazini kujitenga na kusini mwaka 2011.
Ziara hii ya kwanza ya Deng nchini sudan akiwa makamo wa raisi inakuja makuma kadhaa baada ya kuteuliwa kushika nafasi ya aliyekuwa kiongozi wa waasi Riek Machar kufuatia ghasia zilizoibuka mjini Juba na kusababisha vifo vya mamia ya watu mnamo mwezi Julai.
Waziri wa mambo ya kigeni wa sudan kaskazini Kamal Ismail amesema kuwa wamempokea Taban Deng kama makamo wa kwanza wa raisi wa taifa la Sudan Kusini.
Wakati Khartoum ikionesha kumtambua Deng kama makamo wa raisi wa sudan kusini mataifa nane yanayounda kanda la IGAD ambayo pia Sudan ni mwanachama bado kutambua uteuzi wake.
Masuala ambayo hayajapatiwa ufumbuzi tangu kujitenga kwa Sudani Kusini ni pamoja na hadhi ya wilaya ya mpakani ya Abyei iliyochukuliwa na Khartoum, ambayo imekuwa ikitakiwa kupiga kura kuhusu hatma yake na malipo ambayo Juba inapaswa kufanya kwa kutumia bomba la mafuta kusafirisha mafuta nchini Sudan.RFI

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger