TRA

TRA

Tuesday, August 2, 2016

SERIKALI YAWAJENGEA UWEZO WATENDAJI WAKE

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


1
Mkurugenzi  wa Mikataba, Ofisi ya  Mwanasheria  Mkuu wa  Serikali Bi. Eveline Makala  akitoa neno la ukaribisho  kwa washiriki wa nafunzo (hawapo pichani) 
2
Washiriki wa  mafunzo  wakifuatilia  Mada ya dhana ya ubia iliyokuwa  ikiwasilishwa  na Dkt  Frank  Mshiru kutoka Wizara ya  Fedha na Uchumi 
Na Mwandishi wetu
Serikali ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania imeendelea kuwajengea uwezo watendaji wake ili kuwawezesha kuhakiki na kusimamia utekelezwaji wa miradi ya uwekezaji ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi (Public Private Partnership) katika sekta ya Nishati na madini.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa watendaji mbalimbali wa Serikali yanayofanyika kuanzia Agosti 1-4,2016 mkoani Tanga, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ndugu Gerson Mdemu ameeleza kuwa Serikali imechukua hatua hiyo ili kuondoa ombwe la uelewa wa watumishi wa umma kuhusu Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi ya mwaka 2010  (The Public Private Partnership Act).
Itakumbukwa kuwa, kabla ya mwaka 2010,hakukuwa na Sheria iliyosimamia huduma itolewayo na ubia kati ya Sekta ya umma na Sekta binafsi ingawa tayari kulikuwa na huduma ambazo zilikuwa zikitolewa kwa sura ya ubia kati ya mashirika ya dini na serikali au mashirika ya umma katika sekta ya afya,elimu na maji jambo ambalo lilipelekea Serikali kutumia gharama kubwa katika kuhakikisha kuwa miradi husika inatekelezwa ipasavyo.
Ili kuondokana na changamoto hiyo, Serikali ililazimika kurasimisha shughuli zilizokuwa zikifanywa na sekta binafsi katika utoaji wa huduma kwa umma kwa kutunga Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya umma na sekta binafsi kwa lengo la kutumia teknolojia na utaalamu wa sekta binafsi kutoa huduma yenye gharama nafuu kwa umma na kuhakikisha kuwa huduma inayotolewa na sekta binafsi inaendana na vigezo vilivyowekwa na Serikali.
Aidha Ndugu Mdemu alifafanua kuwa Sheria hii imeipa Sekta binafsi njia mbili za utoaji huduma ambazo ni  mosi, kujenga miundombinu mipya na bora na pili ni kumiliki miundombinu ya Serikali, kuiboresha na kuiendesha wakati wa kutoa huduma bora na kuikabidhi Serikalini baada ya muda wa mkataba kukamilika.
Vilevile Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametumia fursa hiyo kuzikumbusha taasisi za Serikali kuzingatia ushauri wa kisheria unaotolewa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika utekelezaji wa mikataba na majukumu mbalimbali kama ilivyoainishwa katika kifungu cha 23 cha Sheria ya Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ya mwaka 2005 (The Attorney General [Discharge of Duties] Act) ambacho kinaeleza kuwa ushauri unaotolewa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndio msimamo wa Serikali hadi utakapoondolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali mwenyewe au Mahakama.
“Kwa Mawakili wa Serikali,umuhimu wenu unatokana na nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama ilivyowekwa wazi Kikatiba. Mwanasheria yeyote wa Wizara,Taasisi,Mashirika ya Umma au Serikali za mitaa anayetoa ushauri wa kisheria katika eneo lake la kazi,kimsingi anafanya kazi kwa niaba ya Mwanasheria Mkuu” aliongeza Ndugu Mdemu.
Naye Mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Dkt Mhiru    alieleza kuwa washiriki watajengewa uwezo wa masuala muhimu ya kuzingatia wakati wa kuhakiki mikataba ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ili kuiwezesha nchi kupiga hatua katika ukuaji wa uchumi .
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mikataba kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Bi Evelyne Makala alieleza kuwa sekta ya Nishati ni sekta ambayo ina mikataba mingi ya ubia na yenye maslahi makubwa kwa Taifa hivyo mafunzo haya yatasaidia katika kutoa mwongozo wa uhakiki na kusimamia miradi ya uwekezaji katika sekta ya Nishati na madini.
Mafunzo hayo amabayo yamefadhiliwa na Shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) yameshirikikisha watendaji wa Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu,Wizara ya Nishati na Madini,Wizara ya Fedha na Mipango,Wizara ya Mambo ya Nje,Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kimataifa, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Zanzibar,Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa Jamhuri ya Muungano,na watumishi kutoka Ofisi za Mwanasheria Mkuu za Mikoa ya Pwani,Arusha,Morogoro,Tanga na Ofisi ya Wilaya ya Monduli. (P.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger