Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa Michezo akichangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016
ambapo alisema Muswada huu utasaidia kuongeza uwazi na uwajibikaji pia
utasaidia kukuza tasnia ya habari nchini, Wakati wa Kikao cha 2 jana
Bungeni Mjini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) akichangia akichangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa
ya mwaka 2016 ambapo alisema Muswada huu utasaidia kukidhi hitaji la
kikatiba la watu kupata taarifa, Wakati wa Kikao cha 2 jana Bungeni
Mjini Dodoma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akichangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016
ambapo alisema na kusisitiza umuhimu wa muswada huu ikiwemo kuongeza
wigo wa upatikanaji wa taarifa kwa waandishi wa habari.
Waziri wa
Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe akijibu hoja zilizotolewa na
wabunge kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016
ambapo aliwataka wabunge kuacha kupotosha kuwa muswada huu utavibana
vyombo vya habari na kuwataka kuusoma na kuuelewa muswada huo
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO (P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment