Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Badhi ya Mawaziri na viongozi wa
mkoa wa Dodoma baada ya kukagua ujenzi wa makazi mapya ya Waziri Mkuu
kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma Septemba 7,2016. Katikati ni mkewe
Mary.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kulia kwake ) wakikagua ujenzi wa
makazi mapya ya Waziri Mkuu kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma
Septemba 7, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kulia kwake ) wakikagua ujenzi wa
makazi mapya ya Waziri Mkuu kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma
Septemba 7, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu,Kassim Majaliwa na Mkewe Mary (kushoto) wakipata maelezo kutoka
kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana,
Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama kuhusu ujenzi wa makazi mapya ya
Waziri Mkuu, kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma Septemba 7, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kulia kwake ) wakikagua ujenzi wa
makazi mapya ya Waziri Mkuu kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma
Septemba 7, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amefanya ziara ya kukagua ujenzi wa makazi mapya ya
Waziri Mkuu katika eneo la Mlimwa na kuagiza umalizike kwa wakati ili
aweze kuhamia kama alivyoahidi.
Katika
ziara hiyo aliyoifanya leo mchana (Jumatano, Septemba 7, 2016) Waziri
Mkuu amesema ameridhishwa na namna kazi ya ujenzi inavyofanyika.
“Nimekuja
kukagua makazi mapya na mahali pa kufanyia kazi. Kazi ya ujenzi
inaendelea vizuri, nimejionea mwenyewe na naamini katika kipindi kifupi
watakuwa wamekamilisha,” amesema.
Amesema
kutokamilika kwa ujenzi huo hauwezi kukwamisha azma yake ya kuhamia
Dodoma kwa sababu tayari inafahamika kuwa Makao Makuu ya Ofisi ya Waziri
Mkuu yako Dodoma.
Amesema
uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma hautokani na shinikizo la kisiasa bali
ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao chimbuko
lake ni agizo lililotolewa Oktoba Mosi, 1973 kwenye Mkutano Mkuu wa 16
wa chama cha TANU.
“Tangu
wakati huo Serikali zote ziliendelea kufanya juhudi mbalimbali za
kuandaa miundombinu na hata awamu ya nne ilisimamia kwa kiwango kikubwa
uwekaji wa miundombinu hiyo,” amesema.
“Pia
tukumbuke kauli ya Mheshimiwa Rais aliyotoa kwenye hotuba yake ya Julai
23, 2016 alipochaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa CCM, na akairudia tena
Julai 25, kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa na mimi siku hiyo
hiyo nikaweka msisitizo,” amesema.
Amesema
uamuzi wa Serikali ya awamu ya tano wa kuhamia Dodoma unakuja baada ya
kuridhishwa na ujenzi wa miundombinu na maeneo ya kutolea huduma za
kijamii kwa wageni na wenyeji ikiwemo Hospitali ya Benjamini Mkapa
iliyopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yenye uwezo wa kutibu
magonjwa makubwa kama ya moyo na figo.
Waziri
Mkuu amesema tayari Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) ina
mpango kamambe (master plan) na ina viwanja vya kutosha kujenga makazi
na ofisi mbalimbali.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
DODOMA.
JUMATANO, SEPTEMBA 7, 2016.(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment