TRA

TRA

Tuesday, September 6, 2016

TBL Group yafanikisha usalama kituo cha watoto wenye ulemavu

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


tl1
Meneja mawasiliano ya ndani wa kampuni ya TBL group,Zena Tenga (wa kwanza kulia) akisalimia na watendaji wa kituo  kulelea watoto walemavu cha Human Dream Children Village,Emanuel Komba kushoto ni mama mlezi wa kituo hicho,Celina Fransis na kulia ni Meneja wa mawasiliano ya nje wa kampuni hiyo Amanda Walter
tl2
Meneja mawasiliano ya ndani wa kampuni ya TBL group,Zena Tenga (wa pili kulia) akimkabidhi moja ya kiroba cha chupa zilizovunjika kwa ajili ya ujenzi wa uzio Mkurugenzi msaidizi wa Kituo cha kulelea watoto walemavu cha Human Dream Children Village,Emanuel Komba kushoto ni mama mlezi wa kituo hicho,Celina Fransis na kulia ni Meneja wa mawasiliano ya nje wa kampuni hiyo Amanda Walter
tl3
Mkurugenzi msaidizi wa kituo cha kulelea watoto walemavu Human Dream Children Village,Emanuel Komba akiwaonyesha mazingira ya kituo hiko baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TBL group kutembelea kituo hiko na kukabidhi msaada wa vipande vya chupa vya kutengenezea uzio wa kituo hicho
tl4
Mkurugenzi msaidizi wa kituo cha kulelea watoto walemavu Human Dream Children Village,Emanuel Komba(kulia) akiwaonyesha mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo hicho baada ya baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TBL group kutembelea kituo hiko na kukabidhi msaada wa vipande vya chupa vya kutengenezea uzio wa kituo hicho
Kituo cha kuwahudumia watoto wenye ulemavu  cha Human Dream Children Village kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam, ambacho kimekuwa kikikabiliwa na changamoto ya matukio ya wizi kimepata msaada wa vipande vya chupa kwa ajili ya kuimarisha uzio wake kutoka kampuni ya TBL Group.
Msaada huo kwa kituo hicho ni moja ya mkakati wa kampuni ni moja ya mkakati wa kampuni wa kutekeleza kanuni ya afya na usalama ambayo mbali na kulenga maeneo ya kazi inalenga pia kwa jamii kwa ujumla.
Meneja Mawasiliano wa TBL Group,Zena Tenga,alisema kuwa moja ya sera ya kampuni inatoa kipaumbele kutekeleza suala la Afya na Usalama kuanzia kwa wafanyakazi ,wageni wanaotembelea viwanda vyake,wateja  na jamii kwa ujumla.
“Kutokana na sera ya Afya na Usalama tumeguswa na tatizo la kituo hiki la kutokuwa na usalama  ndio maana tumeamua kuwaletea vipande hivi vya chupa vya kuweka kwenye  kwenye uzio kwa ajili ya kuimarisha usalama.Vilevile moja ya mkakati wa kampuni ni kuunga mkono jitihada za serikali za kukabiliana na changamoto mbalimbali  za kijamii”.Alisema  Tenga.
Kwa upande wake Msimamizi Msaidizi wa kituo hicho Emmanuel Komba,ameishukuru kampuni ya TBL msaada huo ambao alidai utasaidia kuondokana na changamoto ya matukio ya wizi na kuhatarisha usalama wa watoto wanaoishi kituoni hapo. “Tunashukuru kwa msaada huu mkubwa kwa kuwa utasaidia kuimarisha hali ya usalama hapa kituoni”.Alisema Komba. (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger