Mwenge wa
uhuru ukikimbizwa kwenye Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara ambapo
ulizindua miradi yenye thamani ya zaidi ya sh1 bilioni.
Mkimbiza
mwenge kitaifa Lucia Kamafa akimtwisha ndoo ya maji Mariam Mollel mkazi
wa Gunge Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ambpo ukiwa Mkoani humo
ulitembelea miradi yenye thamani ya sh7.7 bilioni.
Wakazi
2,986 wa Kijiji cha Endanachan Wilayani Babati Mkoani Manyara, waliokuwa
wanakabiliwa na tatizo la uhaba wa maji, wameondokana na changamoto
hiyo baada ya kuzinduliwa mradi wao utakaozalisha lita 144,000 kwa siku.
Akizindua
mradi huo, kiongozi wa mbio za mwenge uhuru kitaifa George Mbijima
aliwataka wakazi hao kuuchunga na kuutunza mradi huo kwani serikali
imetumia gharama kubwa hadi kufanikisha kuwapatia maji wananchi wake.
Mbijima
alisema maji ni hitaji kubwa la jamii hivyo itakuwa jambo la ajabu
endapo baada ya muda mfupi, miundombinu ya mradi huo ukaharibika kwani
haitakuwa sifa nzuri kwa jamii kususiana na tukio hilo.
Ofisa
mtendaji wa kijiji cha Endanachan Amos Gurti alisema mradi hadi
kukamilika mradi huo umegharimu sh286 milioni, ikiwemo sh29 milioni za
wananchi, sh600 milioni za halmashauri na sh256 milioni za wahisani wa
Water aid na Kanisa katoliki jimbo la Mbulu, (DMDD).
Alisema
kupitia mradi huo wananchi wengi zaidi watapata huduma bora kwani una
vituo tisa vya kuchotea maji ya bomba, bomba za usafirishaji kilometa
1.2 bomba za usambazaji kilometa 7.1 na tenki moja lenge ujazo wa lita
50.
“Usimamizi
na uendeshaji wa mradi huu unategemea zaidi mapato yanayotokana na
ankara za maji yanayochotwa na wananchi wa hapa ambapo ndoo moja ya maji
yenye ujazo wa lita 20 huuzwa kwa sh25,” alisema Gurti.
Mmoja
kati ya wakazi hao Martha Lowri alisema awali walikuwa wanatembea umbali
mrefu kwa ajili ya kufuata huduma ya maji ila baada ya huduma hiyo
kuanzishwa watakuwa wamerahisishiwa kazi ya kufuata maji mbali.
Lowri
alisema hivi sasa hata mahusiano yao ya ndoa kwenye nyumba za wanawake
wa eneo hilo utakuwa mzuri kwani hawatatembea tena umbali mrefu kwa
ajili ya kufuata huduma hiyo mbali na majumbani mwao. (P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment