Naibu
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-Utumishi na Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora Bi. Susan P. Mlawi akisisitiza jambo kuhusu Mpango
Kazi wa Kuendesha Shughuli za Serikali kwa Uwazi ( OGP) wa Awamu ya
Tatu wakati wa mkutano wa wadau wa kujadili mpango huo, uliofanyika jana
katika ukumbi wa mikutano Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa TWAWEZA Bw. Aidan Eyakuze akichangia mada katika mkutano wa
wadau wa kujadili Mpango Kazi wa Kuendesha Shughuli za Serikali kwa
Uwazi (OGP) wa Awamu ya Tatu, uliofanyika jana katika ukumbi wa
mikutano Ikulu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya
wadau waliohudhuria mkutano wa kujadili Mpango Kazi wa Kuendesha
Shughuli za Serikali kwa Uwazi ( OGP) wa Awamu ya Tatu wakimsikiliza
Katibu Mkuu Ikulu Bw. Peter Ilomo (hayupo pichani) wakati akiwasilisha
hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki
(Mb) uliofanyika jana katika ukumbi wa mikutano Ikulu jijini Dar es
Salaam.
Katibu Mkuu Ikulu Bw. Peter Ilomo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano wa kujadili Mpango Kazi wa Kuendesha Shughuli za Serikali kwa Uwazi ( OGP) wa Awamu ya Tatu uliofanyika jana katika ukumbi wa mikutano Ikulu jijini Dar es salaam. Bw. Ilomo alifungua mkutano huo kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (MB).(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment