Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akipokea Salaam ya
heshima kutoka Gwaride Maalum la heshima lililoandaliwa na askari
wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi
Namba 11. Hafla ya hiyo imefanyika leo Januari 13, 2017 katika Viwanja
vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga,
Jijini Dar es Salaam(kushoto) ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo
Dkt. Juma Malewa .
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akikagua Gwaride
Maalum la heshima lililoandaliwa na Askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya
Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kama inavyoonekana
katika picha.
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimtunuku cheti cha
sifa Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha
Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 ambapo Mafunzo hayo yamefungwa rasmi leo
Januari 13, 2017 katika Viwanja vya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia
Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akimvisha nembo ya
kijani Mmoja wa askari wahitimu wa Mafunzo Maalum ya Kikosi Maalum cha
Jeshi la Magereza Kozi Namba 11 kwa niaba ya wahitimu wenzake. Mafunzo
hayo Maalum yamefungwa rasmi leo Januari 13, 2017 katika Viwanja vya
Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani kilichopo Ukonga, Jijini
Dar es Salaam.(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment