TRA

TRA

Friday, March 10, 2017

Erdogan na Putin kukutana Moscow

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Rais wa Urusi Vladmir Putin amepangiwa kukutana na kiongozi mwenzake wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan mjini Moscow hii leo kujadiliana kuhusu vita vinavyoendelea nchini Syria pamoja na kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili.Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ikulu ya Kremlin.Urusi na Uturuki nchi ambazo zinaunga mkono pande tafauti zinazopingana katika vita nchini Syria zimekuwa zikijaribu kujenga upya mahusiano yao katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni baada ya ndege ya kivita ya Uturuki kudungua ndege ya kijeshi ya Urusi katika anga ya mpaka wa Syria na Uturuki mwishoni mwa mwaka 2015. Mkutano huo unakuja baada ya rais Putin hapo jana kukutana na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na kuzungumzia mgogoro huo wa Syria na juhudi za kupambana na ugaidi wa Kimataifa na hasa kundi linalojiita dola la Kiislamu

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger