Watu kadhaa wamejeruhiwa vibaya katika ghasia zilizotokea mbele ya
ubalozi wa Uturuki mjini Brussels, Ubelgiji jana.
Rabsha hizo zimetokea wakati wafuasi na wapinzani wa Rais Recep Tayyip Erdogan waliposhambuliana.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani, watu wanne wamejeruhiwa na Wakurdi watatu wamechomwa kisu na wafuasi wa Rais Erdogan kabla ya polisi kuingilia kati mzozo huo. Waziri Mkuu wa Ubelgiji, Charles Michel amelaani ghasia hizo akisema serikali ya Ubelgiji haitovumilia kabisa ghasia zinazotokana na kura ya maoni nchini Uturuki, yenye lengo la kumpa madaraka zaidi Rais Erdogan. Kura hiyo ya maoni itafanyika Aprili 16.
Rabsha hizo zimetokea wakati wafuasi na wapinzani wa Rais Recep Tayyip Erdogan waliposhambuliana.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani, watu wanne wamejeruhiwa na Wakurdi watatu wamechomwa kisu na wafuasi wa Rais Erdogan kabla ya polisi kuingilia kati mzozo huo. Waziri Mkuu wa Ubelgiji, Charles Michel amelaani ghasia hizo akisema serikali ya Ubelgiji haitovumilia kabisa ghasia zinazotokana na kura ya maoni nchini Uturuki, yenye lengo la kumpa madaraka zaidi Rais Erdogan. Kura hiyo ya maoni itafanyika Aprili 16.
No comments:
Post a Comment