TRA

TRA

Tuesday, April 11, 2017

Japan yatafakari kuwa na uwezo wa kushambulia kutokana na kitisho kutoka Korea kaskazini

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Waziri Mkuu Shinzo Abe  
 
Wakati Korea Kaskazini ikiendelea kufanya majaribio ya makombora ya masafa ya kati, chama tawala nchini Japan cha waziri mkuu Shinzo Abe kinatafakari kujenga uwezo wa kushambulia vituo vya adui. 
Korea Kaskazini hivi karibuni imeimarisha progamu zake za nyuklia na makombora, ambapo katika mwaka uliopita pekee ilifanya majaribio mawili ya nyuklia na mengine 20 ya makombora ya masafa marefu. 
Mapema mwezi Machi Pyongyang alifanya majaribio ya makombora manne, ambapo matatu kati yake yaliangukia katika eneo la bahari linalomilikiwa na Japan. 
Waziri wa zamani wa ulinzi wa Japan Itsunori Onodera anaanimini Korea Kaskazini makombora yenye uwezo mkubwa. 
Waziri mwingine wa zamani wa ulinzi Jenerali Nakatani, alikaribisha hatua ya Marekani kuweka mfumo wa ulinzi dhidi ya makombora nchini Korea Kusini na kuongeza kuwa ni muhimu kusihirikiana na mataifa hayo mawili ili kushghulikia kitisho kinachoongezeka cha Korea Kaskazini.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger