
Manchester United itamkosa mshambulizi wake nyota, Zlatan Ibrahimovic hadi mwaka 2018.
Zlatan
aliumia katika mechi ya Europa baada ya kuruka juu, wakati anatua mguu
wake ulipinda kwenda nyuma.Imeelezwa ameumia misuli mikubwa ambayo
imechanika katika goto la mguu wake wa kulia.Hizi ni habari mbaya kwa
mashabiki wote wa Man United kumkosa mkongwe huyo kwa kuwa katika msimu
wa kwanza tu alishafunga mabao 28.
Siku yake ya kutimiza miaka 36, mwezi Oktoba, mwaka huu itamkuta Zlatan akiwa na nje.
SHARE
No comments:
Post a Comment