TRA

TRA

Monday, April 24, 2017

Upasuaji wa kupandikiza kichwa unatarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza mwaka 2017

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


DESEMBA  2017 inatarajiwa kuwa siku ya kihistoria kwenye sekta ya afya na tiba duniani ambapo utafanyika upasuaji wa kupandikiza kichwa kwa mara ya kwanza utakaofanyika mjini London ikihusisha madaktari 150 na itachukua zaidi ya saa 34.
Kwa mujibu wa Daktari atakayeongoza upasuaji huo Dr. Sergio Canavero, upasuaji huo utafanyika kwa mara ya kwanza kwa binadamu ambapo kichwa cha binadamu aliye hai kitapandikizwa kwenye mwili wa mtu aliyekufa na binadamu huyo kuweza kupata mwili mpya.
Madhumuni ya upasuaji huu ni kusaidia watu waliopata magonjwa ya kupooza viungo, watu wenye vilema vya miguu na magonjwa ya uti wa mgongo kupata matumaini mapya ya kuwekewa mwili mwingine. Upasuaji huu unatajwa kugharimu zaidi ya Dollar millioni 30.
Upasuaji utafanywa kwa mara ya kwanza kwa mgonjwa Valery Spiridonov kutoka Urusi ambaye kitaondolewa kichwa chake na kupandikizwa kwenye mwili wa mtu aliyekufa. Valery Spiridonov amejitolea kufanyiwa upasuaji huou kwa sababu ana tatizo la uti wa mgongo liliopelekea mwili wake kupata ugonjwa wa kiharusi.
VIDEO:Ulipitwa na huu utafiti kuhusu dawa ya uzazi wa mpango ya panya kutumika kwa binadamu?Bonyeza play kutazama



Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger