TRA

TRA

Monday, April 24, 2017

Tujitafakari kabla ya kuridhia maazimio

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Julian Msacky

KWA muda mrefu sasa tunaridhia maazimio mbalimbali ya kimataifa, lakini utekelezaji wake unakuwa wa kusuasua.

Tatizo hili halipo tu hapa kwetu bali linahusu nchi karibu zote za dunia ya tatu na hivyo kukwama kimaendeleo.

Wakati tukisuasua kiutekelezaji Umoja wa Mataifa (UN) unaendelea kuchanja mbuga kwa kuanzisha malengo mengine

   Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guterres

Kwa mfano, hivi sasa umoja huo umezindua Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Malengo hayo yamepatikana baada ya
kumalizika kwa Mpango wa Maendeleo ya Milenia (MDGs).

Hebu tujiulize malengo yaliyokuwa katika mpango huo wa MDGs ulidumu kwa miaka 15 yalitimia kama ilivyotakiwa?

Chini ya MDGs tulitakiwa tuwe tumemaliza umaskini, lakini tatizo hilo linaendelea kwa kasi kubwa na ufumbuzi wake ni bado.

Tunafahamu kuwa umaskini ndiyo adui mkubwa wa maendeleo. Mwenye tatizo hilo hawezi kulima inavyotakiwa.

Mwenye umaskini hawezi kutunza afya yake inavyotakiwa na pia hana ubavu wa kufuta ujinga kwani hana hili wala lile.

Maskini hana habari za kutunza mazingira, mwenye umaskini hana uhakika wa kuwa na makazi bora. Ni tatizo kweli kweli.

Kwa hiyo tunapozungumzia malengo ya maendeleo endelevu ni lazima tuhakikishe watu wanaondokana na umaskini.

Bila kufanya hivyo tutaanzisha mipango lukuki bila mafanikio. Ushauri wangu ni muhimu tuwe makini kuridhia maazimio.

Endapo tumejiridhisha kuwa MDGs hatukufanya vizuri hatuna sababu ya kuridhia maazimio mengine ya UN.

Nalisema hili si kwa nchi yangu tu bali na mataifa mengi ya Afrika kwani tatizo lililopo Tanzania lipo pia Msumbiji.

Ni heri nchi zetu ziwe wazi kwa UN badala ya kuendelea kusonga mbele wakati maazimio ya nyuma hayakufanyikiwa.

Nikiangalia ni nchi ngapi za Afrika zimefanikiwa kumaliza tatizo la umaskini katika malengo ya MDGs sioni.

Kutunza mazingira na kupunguza vifo vya wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano bado lipo tu.

Ndiyo maana Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya
akina Mama na Uzazi Tanzani
Profesa Andrea Pembe
anasema takwimu zinaonesha
akina mama 556
kati ya wajawazito 100,000
hufariki wakati wa ujauzito
na kujifungua kila mwaka.

Idadi hii bado ni kubwa kama alivyokiri Waziri mwenye dhamana ya afya, Ummy Mwalimu hivi karibuni.

“Kwa bahati mbaya nchi
yetu bado, ukiangalia takwimu
zilizotolewa Desemba
mwaka jana, bado tuna idadi
kubwa ya vifo vya uzazi
kwani takriban kila wanawake
100,000 wanaojifungua,
wanawake 556 hufariki,”anasema.

Kwa maana hiyo elimu ya afya uzazi inahitajika kwa kiwango kikubwa ili kuokoa maisha ya mama zetu.

Kama anavyosema Prof Pembe kuwa,“ jamii kama itaelewa nyakati
za hatari wakati wa ujauzito
na kujifungua itakuwa rahisi
kuchukua hatua mapema kwa
kwenda kwenye kituo cha
afya na kuepuka vifo,”.

Ifike mahali tuondokane na vifo hivyo kwa kuhakikisha tunawekeza vya kutosha katika masuala ya afya.

Tunapozungumzia malengo ya maendeleo endelevu maana yake huduma za kijamii zinatakiwe ziwe bora na uhakika.

Ndiyo maana ya endelevu. Lakini haiwezi kuwa endelevu kama watu hawana uhakika wa maji safi na salama.

Hawana uhakika wa afya bora. Hana umeme wa uhakika na badala yake wanaparamia misitu ili waweze kuishi.

Maendeleo endelevu ni dhana pana na kwa sababu hiyo nchi yetu ni lazima isimame imara kuangalia vipaumbe muhimu.

Ni wakati muafaka kutilia mkazo elimu ya afya kuanzia shule za msingi. Muhimu hapa ni kuvunja ukimya.

  

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger