TRA

TRA

Monday, May 29, 2017

Man City wakaribia kumchukua kipa wa Benfica Ederson Moraes

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Manchester City wanakaribia kumnunua kipa wa mabingwa wa ligi ya Ureno Benfica Ederson Moraes kwa jumla ya £33m.

Meneja wa City Pep Guardiola amekuwa akimtafuta mchezaji huyo wa Brazil kwa muda na sasa amepata nafasi baada ya kumwachilia kipa wa klabu hiyo Willy Caballero Ijumaa.

Baada ya ushindi wa 2-1 katika fainali ya Kombe la Ligi nchini Ureno, Moraes alisema kuna uwezekano hiyo ikawa ilikwua mechi yake ya mwisho kuwachezea benfica.




 Ederson alisaidia Benfica kushinda Kombe la Ureno mara ya 26 Jumapili kwa kulaza Vitoria Guimaraes 2-1 

Taarifa zinasema Guardiola pia anataka kumnunua beki wa kati Mfaransa anayechezea Monaco Benjamin Mendy, 22.

Baada ya kukosa kushinda kikombe chochote msimu wake wa kwanza kama meneja City, Guardiol amepanga kufanyia mabadiliko makubwa kikosi cha klabu hiyo kabla ya msimu ujao kuanza.
Pep alichukua hatua ya kwanza wka kumnunua kiungo wa Monaco, Mreno Bernardo Silva kwa £43m Ijumaa.

Caballero ni miongoni mwa wachezaji watano wa City ambao mikataba yao imefikia kikomo na wameruhusiwa kuondoka.
Mshambuliaji Kelechi Iheanacho anatafutwa na West Ham.

Hatima ya wachezaji wanne ambao Guardiola aliwaruhusu waondoke Etihad kwa mkopo msimu uliopita - Joe Hart, Samir Nasri, Wilfried Bony na Eliaquim Mangala - haijabainika
Kuwasili kwa Ederson kutamuongezea presha Claudio Bravo

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger