Mikataba ya
mabilioni ya madola kati ya Marekani na Saudia itatiwa saini siku ya
Jumamosi wakati ambapo rais Trump anafanya ziara yake ya kwanza ya
kigeni Saudia.
Swala kuu linalotarajiwa kuzungumziwa kwenye kikao hicho ni vipi kukabliana na itikadi kali zinazosababisha vitendo vya kigaidi.
Ziara hiyo ya siku nane pia itashirikisha Israel, Palestina,Ubelgiji,Vatican na Sicily.
Ziara hiyo inajiri wakati ambapo bwana Trump anakabiliwa pigamizi kali nchini mwake kufuatia hatua ya kumfua kazi mkurugenzi wa shirika la FBI James Comey.
Amekosoa vikali uamuzi wa kumteua mtaalam kuchunguza ushawishi wa Urusi katika uchaguzi wa Marekani.
Bwana Trump anaandamana na mwanawe Ivanka,mshauri wa ikulu ya Whitehouse pamoja na mumewe Jared Kushner ambaye ni mwanamacha muhimu wa baraza la mawaziri la rais Trump
Kama waziri mkuuwa wa Uingereza Theresa May na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel kuhusu ziara zao za hivi karibuni nchini Saudia, bi Trump na Ivanka hawakuvaa hijab.
CHANZO: BBC
SHARE
No comments:
Post a Comment