• About
  • Services
  • Products
  • Blog
  • Contact Us

NCHI YANGU

Menu
  • Home
  • Lifestyle
    • Sub Menu 1
    • Sub Menu 2
    • Sub Menu 3
  • Sports
    • Sub Menu 1
      • Sub Menu 1
      • Sub Menu 2
      • Sub Menu 3
    • Sub Menu 2
    • Sub Menu 3
  • Post
  • Fitness
  • Music
  • Travel
  • Politics
  • Beauty

TRA

TRA

Wednesday, May 24, 2017

Home > > TTB: Tembeleeni vivutio vya utalii

TTB: Tembeleeni vivutio vya utalii

at 4:03 AM
Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imetoa wito kwa Watanzania kupenda kutembelea vivutio vya utalii vya ndani kwa lengo la kukuza na kuinua pato la Taifa.

Wito huo ulitolewa jana na Ofisa Uhusiano Mkuu wa Bodi ya Utalii, Geofrey Tengeneza alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya kuhusiana na kampeni ya kuhamasisha utalii wa ndani iliyozinduliwa mkoani Mbeya.

Tengeneza alisema Bodi ya Utalii ilifanya utafiti mwaka 2006 na kubaini kuwa idadi kubwa ya Watanzania hawatembelei vivutio vya Utalii vya ndani na badala yake wanajua kazi ya Utalii ni ya wageni kutoka nje ya Nchi.

Alisema baada ya kugundua uwepo wa changamoto hiyo Bodi ilianzisha kampeni mbali mbali za kuhamasisha utalii wa ndani mwaka 2007 ambapo idadi ilianza kuongezeka kutoka watalii 250,000 hadi zaidi ya 800,000 sasa.



Geofrey Tengeneza
Twiga

Alisema matarajio ya Bodi ni kuona utalii wa ndani unaingiza pato kubwa kwa Taifa bila kutegemea Utalii wa Kimataifa hivyo kuendelea kuendesha kampeni zingine zaidi.

Alisema kutokana na kuonekana Wananchi bado wanahitaji elimu zaidi kuhamasishwa kutembelea vivutio vya utalii vya ndani Mei 3, mwaka huu Bodi ilizindua kampeni mpya.

Aliitaja kampeni hiyo ambayo ilizinduliwa katika Mkoa wa Kigoma na kuendelea katika mikoa minne kuwa ni “Utalii wa ndani uanze na mtanzania mwenyewe”.

Aliongeza kuwa baada ya kuzindua kampeni hiyo mkoani Kigoma Bodi ilizindua tena katika Mkoa wa Iringa na sasa Mbeya kisha Mkoa wa Mwanza.

Akizungumzia uzinduzi wa kampeni hiyo katika Mkoa wa Mbeya alisema itafanyika katika viwanja vya Uhasibu kuanzia majira ya saa moja jioni ambapo Agape Television Network(ATN) itakuwa ikionesha matukio ya utalii kupitia skrini kubwa.

Aidha alitoa wito kwa mashirika binafsi kujitokeza katika kuwekeza kwenye miundombinu ya malazi kwenye maeneo yenye vivutio vya Utalii ili kuwavutia watu wanaotembelea.

Alisema kupitia kampeni hiyo mashindano mbali mbali yataendeshwa ambapo washindi watapelekwa kwenye hifadhi za Taifa kutembelea ikiwemo kujishindia zawadi mbalimbali. 

Habari hii imendaliwa na Venance Matinya




Unknown

Author: Unknown

SHARE
  • Share
  • Tweet
  • Share
  • Pin
  • Share
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Fourni par Blogger CodeEnvoyer par emailBlogThis !Partager sur TwitterPartager sur FacebookPartager sur LinkedInÉpingler sur PinterestPartager sur StumbleUponVoter pour cet article sur HelloCoton

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Tupate kupitia Facebook

Popular Posts

  • NEEC FANYENI TATHMINI YA KISAYANSI KUHUSU MANUFAA YA MIFUKO YOTE YA UWEZESHAJI-MAJALIWA
    Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi wa manispaa ya Dodoma, Bw. Godwin Kunambi (wapili kushoto) hundi ya Shilin...
  • MSANII BONGO FLAVA AT MFALME WA MIDUARA BONGO, MR TZ WANOGESHA RAHA ZA PWANI COLLEGE PARK, MARYLAND
    Msanii wa Bongo flava na mfalme wa miduara AT, akiongelea utamaduni wa kiswahili na raha za pwani kwenye jopo la kongamano la rah...
  • TAASISI YA DORIS MOLLEL KWA KUSHIRIKIANA NA CBA WASAIDIA HOSPITALI YA MWANANYAMALA
     Meneja Mahusiano wa  Benki ya CBA, Caroline Makatu (wa pili kushoto)  akikabidhi msaada wa v...

Popular Posts

  • NEEC FANYENI TATHMINI YA KISAYANSI KUHUSU MANUFAA YA MIFUKO YOTE YA UWEZESHAJI-MAJALIWA
    NEEC FANYENI TATHMINI YA KISAYANSI KUHUSU MANUFAA YA MIFUKO YOTE YA UWEZESHAJI-MAJALIWA
    Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mkurugenzi wa manispaa ya Dodoma, Bw. Godwin Kunambi (wapili kushoto) hundi ya Shilin...
  • MSANII BONGO FLAVA AT MFALME WA MIDUARA BONGO, MR TZ WANOGESHA RAHA ZA PWANI COLLEGE PARK, MARYLAND
    MSANII BONGO FLAVA AT MFALME WA MIDUARA BONGO, MR TZ WANOGESHA RAHA ZA PWANI COLLEGE PARK, MARYLAND
    Msanii wa Bongo flava na mfalme wa miduara AT, akiongelea utamaduni wa kiswahili na raha za pwani kwenye jopo la kongamano la rah...
  •  TAASISI YA DORIS MOLLEL KWA KUSHIRIKIANA NA CBA WASAIDIA HOSPITALI YA MWANANYAMALA
    TAASISI YA DORIS MOLLEL KWA KUSHIRIKIANA NA CBA WASAIDIA HOSPITALI YA MWANANYAMALA
     Meneja Mahusiano wa  Benki ya CBA, Caroline Makatu (wa pili kushoto)  akikabidhi msaada wa v...
  • DKT. SHEIN AWAONGOZA VIONGOZI MBALIMBALI KATIKA DUA YA KUMUOMBEA MAREHEMU MZEE KARUME
    DKT. SHEIN AWAONGOZA VIONGOZI MBALIMBALI KATIKA DUA YA KUMUOMBEA MAREHEMU MZEE KARUME
    Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mara alipowasili katika...
  • TRA KUANZA MSAKO MKALI NCHINI
    TRA KUANZA MSAKO MKALI NCHINI
     Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart ikishirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),sambamba na Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa...
  • Mitt Romney asema Trump ni 'tapeli'
    ...

Pages

  • Home
  • About Us
  • Contat Us
 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger