TRA

TRA

Thursday, June 8, 2017

Faru amuua mtunza mazingira Rwanda

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 


Mtunza mmoja wa mazingira ambaye alikuwa akisadia kuwapeleka Faru nchini Rwanda ameuawa na mmoja wa wanyama hao.

Shirika lililoandaa shughuli hiyo la African Parks, lilisema kuwa Krisztian Gyongyi, aliuwawa na Faru, katika mbuga ya taifa ya Akagera alipokuwa akiwafuatilia Faru hao.


 Faru amuua mtunza mazingira Rwanda

Lakini taarifa hiyo haijasema kwa kina jinsi aliuwawa.
Mkurugenzi wa Shrika la Africa Parks Peter Fearnhead, alisema kuwa bwana Gyongyi alikuwa mtu muhimu kawarejesha Faru hao weusi na alikuwa eneo hilo kuwapa mafunzo walinzi wa mbuga jinsi ya kuwafuatilia na kuwalinda Faru
Faru hao walisafirishwa kutoka Afrika Kusini kuenda Rwanda mwezi uliopita.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger