TRA

TRA

Sunday, June 18, 2017

Fifa kujadili pendekezo la kupunguza dakika 90 za mechi

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Shirikisho linaloweka sheria za soka duniani lina mpango wa kupunguza muda wa kipindi cha kwanza na cha pili cha mchezo ili kuwa dakika 30.

Bodi ya kimataifa ya soka duniani itajadili pendekezo hilo linalolenga kupoteza muda unaopotezwa kwa makusudi.

Waliopendekeza mpango huo wanasema kuwa mechi huchezwa kwa dakika 60 pekee kati ya tisini na muda uliosalia hutumiwa kupoteza wakati.

Wanapendekeza dakika 30 kila kipindi huku muda ukisimamishwa kila mpira unapotoka kusaidia kukabiliana na muda unaopotezwa mbali na kuufanya mchezo kuvutia zaidi.

   Mshikemshike uwanjani

Wakosaoji wanasema kuwa mabadiliko kama hayo hayatakuwa na umuhimu wowote iwapo sheria ya kupoteza muda itaimarishwa.
Pendekezo jingine litasababisha wachezaji kutoruhusiwa kupiga mpira mara ya pili baada ya kipa kuupangua wakati wa penalti.

Na iwapo penalti hiyo haikupigwa ilivyotarajiwa ,mchezo utasitishwa na mpira wa adhabu kutolewa.

Mapendekezo mengine yanashirikisha kuweka saa katika uwanja ambayo italingana na ile ya refa mbali na sheria mpya itakayoruhusu mchezaji kujipigia mpira ama hata kutamba na mpira wakati anapopiga mpira wa adhabu.

Tayari aliyekuwa mkufunzi wa Chelsea Gianfranco Zola anapendelea pendekezo hilo la kupunguza muda wa dakika za mechi hadi 60.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger