Jeshi la
Wananchi (JWTZ) limetoa tahadhari kwa umma juu ya matapeli wanaowalaghai
wananchi kwamba watawapa ajira katika jeshi hilo na Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT).
Akitoa
tahadhari hiyo, Mkuu wa Utumishi wa JWTZ, Meja Jenerali Harrison Masebo
amesema wamepokea malalamiko mengi ya wananchi kuhusu utapeli huo na
kusisitiza kwamba jeshi lina utaratibu wake wa kuajiri na siyo kuwatumia
watu wengine kufanya kazi hiyo.
Masebo
amesema wanawatafuta watu hao kwa sababu wanalichafua jeshi kwa kujiita
maofisa wa JWTZ na kujenga dhana kwa wananchi kwamba wametapeliwa na
jeshi.
"Tunaomba
ushirikiano wa wananchi ili tuweze kuwakamata watu hao. Mtu akikwambia
anataka kukupa kazi JKT au JWTZ wewe msikilize lakini tuletee taarifa
kabla hukampa chochote, sisi tutamkamata,"amesema Masebo.
Mkuu huyo
wa utumishi jeshini amesema ajira zote zinazotelewa na JKT lazima
zitangazwe kwenye vyombo vya habari na mchakato wake uko wazi.
Amewataka wananchi wasiwape chochote matapeli hao badala yake watoe taarifa jeshini.
SHARE
No comments:
Post a Comment