Mkuu
wa mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo akikaribishwa na Balozi wa Tanzania
nchini Ufaransa Mhe. Samwel Shelukindo katika ubalozi uliopo jijini
Paris. Gambo yupo katika ziara ya mafunzo nchini Ufaransa, ambapo
pamoja na mafunzo hayo amekuwa akiutangaza mkoa wa Arusha kama kitovu cha
utalii nchini Tanzania.
Mhe
Gambo akiwa huko mefanya mazungumzo na Balozi Shelukindo, na
kubadilishana mawazo ya namna ya kuvutia wananchi wa nchi hiyo
kutembelea Tanzania.
Ufaransa
ni moja ya zinazoleta watalii wengi nchini Tanzania. Pamoja na mambo
mengine Mhe RC na Balozi wamejadiliana mambo ya Msingi ya kufanya ili
kuongeza watalii kutoka Ufaransa kuja Arusha, kupata wawekezaji kutoka
Ufaransa kuja Arusha pamoja na namna ya kutangaza fursa za uwekezaji
zilizopo Mkoani humo, pamoja na kuanzisha tukio la kimataifa la
kutangaza utalii mkoani Arusha kila mwaka.
Mkuu
wa mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo akiweka saini katika kitabu cha
wageni baada ya kukaribishwa na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe.
Samwel Shelukindo katika ubalozi wetu uliopo jijini Paris.
SHARE
No comments:
Post a Comment