Ndege moja ya
shirika la China Eastern Airlines ililazimika kurudi mjini Sydney
Australia baada ya kupatwa na hitilafu wa mitambo ambayo ilisababisha
shimo sehemu ya injini ya ndege hiyo.
Ndege ya MU736 ilikuwa
safarini kutoka Sydney ikilekea Shanghai China lakini rubani akaripoti
kuhusu matatizo kwenyr injini katibu saa moja baada ya ndege kuanza
safari.Abiria waliambia vyombo vya habari kuwa walihisi harufu na kitu kinachochomeka ndani ya ndege.
Ndege hiyo aina ya Airbus A330 ilitua salama na hakukuwa na ripti zozote za majeruhi.
Picha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zilionyesha shimo kubwa upande wa injini.
Abiria kadha walisema kuwa walisikia sauti kubwa ikitokea injini ya upande wa kushoto muda mfupi baada ya ndege kupaa.
Abiria mmoja aliambia shirika la Seven News Network, "ghafla tukaskia sauti hii...kisha tukahisi haribu ya kuchomeka."
CHANZO: BBC
SHARE
No comments:
Post a Comment