.Wanafunzi wa Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam ( DIT) wakimsikiliza kwa makini Afisa Usalama Mwandamizi wa TBL Group Khery Gunzarethy
Mtalaam wa upishi wa bia wa TBL Group Christian Tarimo akiwapatia maelezo ya kitaalamu ya moja ya mchakato wa uzalishaji
Mtalaam wa upishi wa bia wa TBL Group Christian Tarimo akiwaonyesha moja ya mitambo ya uzalishaji wa bia
.Wanafunzi wakisikiliza kwa makini maelezo ya kitaalamu
Wanafunzi wakimsikiliza mtaalamu wa maabara Lyidia Soi
wanafunzi wa DIT katika picha ya pamoja baada ya kufanya ziara ya mafunzo TBL.
……………………….
Wanafunzi
kutoka Chuo Cha Teknolojia Dar Es Salaam (DIT) wamefanya ziara ya
mafunzo katika kiwanda cha TBL cha Ilala na kujionea jinsi TBL Group ilivyojipanga kuwa kioo cha utekelezaji wa sera ya kujenga Tanzania ya Viwanda.
Akiongea na ujumbe wa wanafunzi hao, Afisa Afisa Usalama Mwandamizi wa TBL Group Khery Gunzarethy , alisema kuwa wakati serikali ya awamu ya tano imedhamiria kujenga Tanzania ya Viwanda kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi na
kuongeza fursa za ajira kwa kasi kuna haja ya kuhakikisha kunakuwepo
wataalamu wa kubuni na kuendesha mifumo ya kisasa ya biashara ili
biashara zitakazoanzishwa zizidi kukua na kuwa endelevu.
Gunzarethy Alisema biashara yoyote inayoendeshwa kwa kufuata misingi ya kitaalamu ni lazima ipate mafanikio na kuwa endelevu “Biashara
ikiendeshwa kwa misingi ya kitaalamu inakua kwa haraka na kuchangua
kukuza uchumi wa nchi,kuongeza wigo wa ajira za moja kwa moja na zisizo
za moja kwa moja,kuchangia pato kubwa kwa serikali kwa njia ya kulipa
kodi na kunufaisha jamii kwa namna mbalimbali”.
Aliwaeleza wanafunzi hao kuwa TBL Group kupitia viwanda vyake
vilivyopo kwenye mikoa mbalimbali nchini kwa kiasi kikubwa imekuwa
ikizingatia kuendesha shughuli zake kwa kufuata misingi bora ya
uendeshaji biashara ambayo kwa kiasi kikubwa imewezesha kampuni kupata
mafanikio mengi na kuwa kioo cha uwekezaji bora ambapo watu kutoka
sehemu kadhaa wamekuwa wakitembelea viwanda vyake kwa ajili ya kujifunza
mifumo ya uzalishaji bora wenye tija na ufanisi.
“Kampuni
ya TBL Group imekuwa ikifanya vizuri katika maeneo mbalimbali ikiwemo
kuchangia pato la taifa kwa njia ya kulipa kodi,utunzaji wa
mazingira,kutoa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja
kupitia mtandao wa biashara zake,kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa
wafanyabiashara wadogo inaoshirikiana nao,kuendesha kampeni ya unywaji
wa kistaarabu kwenye jamii,kuwezesha wakulima ambao wanaiuzia malighafi
na imekuwa kinara wa kutekeleza kanuni bora za ajira ambapo imekuwa
ikishikia rekodi ya kupata tuzo ya Mwajiri bora inayotolewa na Chama cha
Waajiri nchini (ATE)”.Alisema.
Aliongeza
kuwa mafanikio haya hayatokani na kufuata mifumo bora ya uzalishaji
pekee bali ni kuwa na wafanyakazi wenye vipaji vikubwa na taaluma
mbalimbali ambao wanafanya kazi kwa kujituma wakati huohuo kampuni ikiwa
inawapatia motisha na mafunzo ya kwa mara ili kuhakikisha wakati wote wanakwenda na wakati sambamba na mabadiliko ya teknolojia yanayotokea siku hadi siku.
Aliwaeleza kuwa TBL Group chini ya kampuni mama ya AbInBev itaendelea kufanya kazi sambamba na serikali,taasisi zingine na wananchi kwa ujumla kwenye jamii kuhakikisha maendeleo
endelevu yanapatikana na aliwaasa wanafunzi kusoma kwa bidii ili wapate
elimu nzuri itakayowawezesha kushindana katika soko la ajira ikiwemo
kujiajiri kupitia taaluma zao
SHARE
No comments:
Post a Comment