TRA

TRA

Friday, June 30, 2017

Venus Wiliams ahusika katika ajali mbaya ya barabarani

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


 
Nyota wa mchezo wa tenisi Venus Williams amehusika katika ajali mbaya ya barabarani iliomuua mwanamume wa miaka 78.

Msemaji wa kituo cha polisi cha Palm Beach Gardens mjini Florida aliithibitishia BBC kwamba walikuwa wanachunguza ajali hiyo iliomuhusisha bingwa huyo wa taji la Grand Slam.

"Mtu mmoja alipelekwa hospitali baada ya ajali hiyo iliofanyika tarehe 9 mwezi Juni na kufariki wiki mbili baadaye kutokana na majeraha ," alisema.

Kulingana na chombo cha habari cha TMZ, ambacho kilitoa habari hiyo, maafisa wa polisi wanaamini kwamba Williams ni wa kulaumiwa lakini wakili wake anasema kuwa ilikuwa ajali.

Nyota wa mchezo wa tenisi Venus Williams amehusika katika ajali mbaya ya barabarani iliomuua mwanamume wa miaka 78.

Mtu aliyefariki ,Jerome Barson, alikuwa akisafiri na mkewe aliyekuwa akiendesha gari hilo kupitia eneo la makutano wakati ajali hiyo ilipotokea.

''Gari la bi Williams lilingia kwa haraka katika barabara yao halikuweza kuondoka kwa haraka kutokana na msongamano wa magari barabarani kulingana na taarifa ya shahidi katika ripoti ya polisi iliopatikana na vyonbo vya habari.

Bi Barson pia alipelekwa hospitalini lakini akapona.
Bi Williams ana makosa kwa kukiuka sheria ya kumpatia heshima dereva aliye na haki ya kupita, ripoti hiyo ilisema, ikiongezea kwamba hakukuwa na maswala mengine kama vile ushawishi wa dawa za kulevya, pombe ama hata kusumbuliwa na simu ya rununu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger