TRA

TRA

Saturday, July 15, 2017

ACACIA YASALIMU AMRI KWA TANZANIA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia imekubali kuilipa serikali ya Tanzania nyongeza ya mrabaa wa kati ya asilimia 4 mpaka 6 kama ilivyoainishwa kwenye muswada wa sheria mpya ya madini nchini humo.

Serikali ya Tanzania na kampuni ya Acacia ziliingia katika mgogoro mapema mwezi tatu mwaka huu kutokana na kuzuiliwa kwa makontena 256 ya Mchanga wa dhahabu (makinikia) kwenye Bandari ya Dar es Salaam baada ya kubainika kuwa Acacia haitoi taarifa sahihi ya kiwango cha madini kilichopo katika mchanga huo hivyo kulipa tozo zisizo sahihi kwa karibu miongo miwili jambo ambalo linapingwa vikali na kampuni hiyo.

Rais Magufuli akihesabu makontena yenye mchanga wenye madini alipofanya ziara ya kushtukiza mwezi Machi
Licha ya kukubali kulipa ongezeko hilo Acacia imesema bado inaendelea kutathimini athari zozote zinazoweza kujitokeza kutokana na kuundwa kwa sheria hiyo mpya.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger