TRA

TRA

Wednesday, July 19, 2017

AJALI HIZI JAMANI, HEBU ANGALIA HAPA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la SULTAN YUSUPH, ambaye alikuwa utingo, mkazi wa Kibaha Mkoani Pwani,amefariki dunia baada ya lori aina ya Howo kupinduka katika Kijiji cha Gumbiro Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma.Lori hilo lililokuwa limebeba makaa ya mawe lilikuwa likitokea Kitai Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma.
 
Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma, GEMINI MUSHY amesema kuwa dereva wa lori hilo amejulikana kwa jina la KAZI YUSUPH na kwamba gari hilo ni mali ya kampuni ya Sun Shine ya Wilayani kibaha mkoa wa pwani na kwamba chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari hilo kuendesha gari kwa mwendo kasi.
 
Kamanda MUSHY amesema hali ya dereva wa gari hilo inaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma kutokana na majeraha aliyoyapata katika sehemu mbalimbali za mwili wake.
Ametoa wito kwa madereva kwamba jeshi hilo litaongeza kasi ya kuwapima kiwango cha ulevi madereva wote ili kuondokana na ajali zinazo sababisha kupoteza maisha ya Watanzania.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger