TRA

TRA

Saturday, July 15, 2017

BEYONCE HATIMAYE APIGA PICHA NA PACHA WAKE

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Beyonce hatimaye amesambaza picha ya kwanza aliyopiga na watoto wake pacha kuadhimisha mwezi mmoja tangu wazaliwe.
Msanii huyo wa Marekani alithibitisha kwamba majina yao ni Sir Carter na Rumi ambayo yalitolewa katika uvumi baada yeye na mumwe kuyatumia kama nembo ya biashara.

Picha hiyo inamuoyesha mama huyo mwenye umri wa miaka 35 na pacha hao wakiwa ndani ya shiti la rangi ya zambarau huku yeye mwenye akiwa amevalia vazi la rangi ya buluu.
.Ilipata watu milioni mbili walioipenda katika mtandao wa Instagram katika saa moja tu.

Beyonce aliandika: Sir Carter na Rumi wamefikisha mwezi mmoja leo huku akiweka emoji ya mikono ya maombi na mwanamke, mwanamume na watoto wawili.




 Beyonce apiga picha na pacha wake

Mbali na pacha hao ambao ni mvulana na msichana Beyonce na JAY-Z pia ni baba wa mtoto wa miaka mitano Blue Ivy. 

Mtindo wa picha hiyo ambapo Beyonce amesimama katika bustani akiwa hana viatu mbele ya eneo lenye maua unafanana na picha aliyopiga akitangaza uja uzito wake katika mtandao huo.

Ulimwengu ulikuwa ukisubiri kwa hamu kuwaona watoto hao tangu vyombo vya habari viliporipoti kwamba mwimbaji huyo wa Lemonade alikuwa amejifungua mwezi uliopita.
Lakini hakuna kati yao aliyethibitisha pacha hao .
Babake Beyonce Martin Knowles alituma ujumbe katika Twitter tarehe 18 mwezi Juni akisema: Ndio hawa 'happy birthday kwa pacha hao''- lakini wakati wa chapisho hilo la Beyonce linaonyesha kuwa watoto hao walizaliwa tarehe 14 mwezi Juni.

Haishangazi kwamba mashabiki walilazimika kusambaza maoni yao katika picha hiyo. DJ wa BBC radio One Clara Amfo aliandika katika Twitter: Soo extra and I love it.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger