TRA

TRA

Monday, July 10, 2017

KIWANDA MALI YA MCHINA KUFUNGWA KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


MPI1
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Joelson Mpina (Mb.) akiongea na baadhi ya wananchi wa mtaa wa Mivinjeni Buguruni Sukita alipowatembelea kufuatia kero ya utiririshwaji wa maji yanayosadikiwa kuwa na  kemikali kutoka katika baadhi ya viwanda maji yanayotumiwa na wakazi wa maeneo hayo kwa kumwagilia bustani za mboga mbonga. Kutoka kulia kwake ni Naibu Meya wa  wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto, Afisa Mazingira Ilala Bw. Adon Mapunda na Diwani wa kata ya Buguruni,  Adam Fugane.
MPI2
Naibu Waziri Mpina Akiongea na Wanahabari katika Bonde Buguruni Sukita jijini Dar es Salaam alipofanya Ziara leo.
MPI3 MPI4
Bwana Jafari Chimgege mratibu wa Mazingira kutoka Baraza la Taifa la usimamizi na Hifadhi ya mazingira NEMC kanda ya mashariki akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Mpina kuhusu Kiwanda cha ANBANGS kinachomilikiwa na raia wa China kivyokaidi kutoa faini ya shilingi milioni 25, iliyotozwa mwaka jana mwezi November kutokana na uchafuzi wa mazingira.
MPI5
Pichani ni  kijana ambaye jina lake halikupatikana akimwagilia maji yanayosadikiwa kuwa na kemikali mbogamboga aina ya majani ya Maboga zinazochipua katika eneo la mtaa wa mivinjeni buguruni sukila, leo. (Habari na Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
…………………………………………………………………….
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limepewa siku saba kukagua na kujiridhisha na uzalishaji, management na utekelezaji wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake kwa Kiwanda cha ANBANGS kinachotengeneza mifuko aina ya viroba vinavyotumika kama vifungashio vya saruji, sukari na aina nyingine ya nafaka, na kukifunga kwa kile kinachodaiwa kukaidi maagizo ya serikali ya awamu ya tano ya kutokulipa faini kwa uchafuzi wa mazingira.
Naibu Waziri Ofisi ya Makmu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina alitoa agizo hilo Leo alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Buguruni baada ya kupata malalamiko yaliyoibuliwa na wakazi wa mtaa wa sukita mivinjeni kupitia kituo cha ITV ambapo  Naibu waziri Mpina alitembelea eneo hilo na kujionena namna ambavyo kiwanda hicho kinavyoendelea kutiririsha maji machafu.
Akiwasilisha taarifa ya ukaguzi wa kiwanda hicho Bw. Jafari Chimgege ambae ni Mratibu wa mazingira kutoka NEMC kanda ya Mashariki alimueleza Naibu waziri Mpina, kuwa “Kama unakumbuka Mhe. Waziri Tulikuja hapa mwaka jana Novemver na tukafanya ziara na ukaguzi hapa na kila tukija hapa hawa wachina wanashindwa kuonyesha ushirikiano na kusema kuwa wao hawajui lugha ya Kiswahili, tuliona makosa mengi na tuliwatoza faini ya shilingi milioni 25, na ilitakiwa walipe ndani ya wiki mbili, lakini Mhe. Hiyo Faini haikulipwa. Na bado wanaendelea na uchafuzi wa mazingira pamoja na kukaidi agizo za serikali.” Alisisistiza Chimgege.
Pamoja na maelezo hayo ya Bw. Chimgege Naibu Waziri alielekeza Baraza hilo kupitia documents zote muhimu zinazohusu, kiwanda hicho ambacho awali hakikuwa na cheti ya tathmini ya athari ya mazingira wala vibali ya aina yoyote ya kutirirsha maji yaliyotibiwa na kuuganishwa na mfumo wa mji taka wa DAWASCO hali ambayo ilimpelekea Mpina pamoja na hilo kuagiza wamiliki wa kiwanda hicho kufikishwa mahakamani
Katika Ziara zake za  ukaguzi wa Mazingira na viwanda jijini Da es Salaam, Mpina amehadi kuingia hatua ya kushirikiana na mamlaka husika kuchukua sampuli za maji yanayopita katika bonde la mto msimbazi katika eneo la viwanda vya karibu na mtaa wa sukita mivinjeni ili kuyafanyia vipimo na kijirisha kama yana madhara kwa viumbe hai na mazingira hususani mboga mboga zinazomwagiliwa maji katika maeneo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger