Jaji mmoja nchini
Marekani amesitisha mnada wa vitu binafsi vya mwanamuziki Madonna baada
ya kusema kuwa haki yake ya faragha ilikiukwa.
Chupi ya Madonna, kitabu cha hundi , kichana , picha na barua ya uhusiano kati ya msanii huyo na aliyekuwa mwanamuziki Tupac Shakur ni miongoni mwa vitu vilivyosimamishwa kupigwa mnada.
Madonna anasema kuwa vitu hivyo viliibwa na rafikiye wa zamani.
- Tupac alidai Madonna alivunja uhusiano wao kwa sababu ya ubaguzi
- Madonna akana madai ya kupanga watoto
- Rihanna amfikia Michael Jackson kwa nyimbo Marekani
Barua hiyo ni ya tarehe 15 mwezi Januari 1995 na iliandikwa na Tupac Shakur wakati alipokuwa akihudumia kifungo cha miezi 18 kabla ya kupigwa risasi na kuuawa. Wasanii wote wawili walikuwa maarufu sana wakati huo.
SHARE
No comments:
Post a Comment