TRA

TRA

Saturday, July 15, 2017

Mwana wa Trump alikutana na Jasusi wa Urusi

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mwana wa Trump Donald Trump JR na Rinat Akhmetshin ambaye alikuwa Jasusi wa Urusi


Aliyekuwa afisa wa kijasusi wa Urusi alihudhuria mkutano mwaka uliopita na maafisa wakuu wa rais Donald Trump na mwanawe ,imebainika.

Rinat Akhmetshin, ambaye sasa ni mkereketwa alithibitisha kwa vyombo vya habari vya Marekani alikuwa katika mkutano huo uliofanyika katika makao makuu ya Trump katika jumba la Trump Tower.

Mwanawe Trump aliahidiwa kupewa habari mbaya dhidi ya mgombea wa chama cha Democrat Hillary Clinton katika mkutano huo , kwa mujibu wa barua pepe zake.

Mwana huyo wa Trump awali alikuwa amekiri kwamba kulikuwa na wakili wa Urusi Natalaia Veselnitskaya aliyehudhuria.
Donald Trump Jr alikuwa amekana kuwepo kwa mkutano uliofanyika tarehe 9 mwezi Juni 2016 , kabla ya kuripotiwa wiki hii.
Lakini kamati ya haki ya bunge la seneti imemtaka mwana huyo mwenye umri wa miaka 39 kutoa ushahidi hadharani.
Majopo kadhaa ya bunge la Congress nchini humo pamoja na majasusi wanachunguza madai kwamba Urusi iliingilia uchaguzi wa Marekani mwaka uliopita ili kumsaidia Donald Trump kuibuka mshindi.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger